Njia rahisi ya kupika ‘half keki’

July 18, 2024 1:53 pm · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link
  • Hamira sio lazima kuweka kwenye half kake.
  • Poza mafuta yako kila baada ya mpiko mmoja.

Watu wengi wanapendelea kupika ‘half keki’ kwa sababu ni pishi ambalo halitumii nguvu nyingi katika uandaaji wake. Pia ni rahisi kupika hata kwa mtu anayeanza kujifunza mapishi.

‘Half keki’ ni kitafunwa kinachotengezwa kwa ngano ambacho wengine hukifananisha na maandazi.

Kumbuka tu chakula hiki ni fursa ya biashara na matumizi ya nyumbani kwa sababu bei yake ni kati ya  Sh500 hadi Sh1,000 katika migahawa mbalimbali. 

Hata hivyo, bei hutofautiana kutoka eneo mmoja kwenda eneo lingine. Faida itategemea na eneo unalofanyia biashara na mapenzi ya watu kwa chakula hicho ambacho hutumiwa zaidi asubuhi kwa chai au juisi.  

Tuingie jikoni

Hatua ya kwanza ni kuchanganya unga wa ngano na vitu vyote (kasoro mafuta ya kuchomea) kisha ukande. Hakikisha unakuwa mgumu ila usiwe kama unatengeneza biskuti. 

Baada ya hapo sukuma na ukate maumbo uyapendayo (hakikisha unakata vipande vinene kiasi na sio kama maandazi) 

Hatua inayofuata ni kuziweka sehemu yenye joto na uache ziumuke kwa dakika 20 hadi 30.

Zikiumuka zikaange katika moto mdogo ili ziive mpaka ndani, kisha ziipue na uweke katika chujio ili kuondoa mafuta.

Mpaka hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa na kinywaji chochote.

Vitu vya kuzingatia

  • Hakikisha unatumia vipimo sahihi bila kusahau ‘baking soda’ 
  • Sio lazima kuweka hamira kwenye ‘half keki’
  • Kanda unga wako uwe mgumu hata kidole kishindwe kupenya.
  • Weka half keki zako kwenye mafuta kabla hayajapata moto.
  • Poza mafuta yako kila baada ya mpiko mmoja, (unaweza kuepua ili yapoe au ukaongeza mafuta ya baridi)
Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Zungu: Kura zimepigwa , pesa ya Serikali imeruhusiwa kuanza sasa kuitumia

Zungu: Kura zimepigwa , pesa ya Serikali imeruhusiwa kuanza sasa kuitumia

Nukta TV

Bunge la Tanzania lapitisha ya Serikali kwa 97%

Bunge la Tanzania lapitisha ya Serikali kwa 97%

Nukta TV

Hawa hapa wabunge waliopiga kura ya hapana, kupitisha Bajeti ya Serikali

Hawa hapa wabunge waliopiga kura ya hapana, kupitisha Bajeti ya Serikali

Nukta TV