Ndege yalipuka Urusi, watu 41 wafariki dunia
- Ndege aina ya Sukhoi Superjet-100 inayomilikiwa na shirika la ndege la Aeroflot la Urusi imewaka moto baada ya kutua kwa dharura katika uwanja wa ndege wa Sheremetyevo katika jiji la Moscow.
- Ilikuwa na abiria 73 na maafisa watano.
Ndege aina ya Sukhoi Superjet-100 inayomilikiwa na shirika la ndege la Aeroflot la Urusi imewaka moto na kuua watu 41 baada ya kutua kwa dharura katika uwanja wa ndege wa Sheremetyevo katika jiji la Moscow.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Urusi, ndege hiyo ilikuwa na abiria 73 na maafisa watano, ambapo kati ya waliofariki ni watoto wawili na mhudumu mmoja.
Video fupi inayosambaa katika mitandoa ya kijamii inaonyesha baadhi ya abiria wakitumia mlango wa dharura na kutoka kwenye ndege hiyo ya Aeroflot iliyokuwa inateketea moto.
     Â
Taarifa ya Aeroflot iliyotolewa jana (Mei 5, 2019) imeeleza kuwa ndege hiyo iliondoka uwanja wa ndege wa Sheremetyevo kutoka eneo la Murmansk lakini baada ya kutua kwa dharurua katika uwanja huo, injini za ndege hiyo ziliwaka moto katika njia kuu wa ndege.
Shirika hilo limesema maafisa hao wa ndege walijitahidi kadri ya uwezo wao kuwaokoa abiria lakini wachache walifanikiwa kutolewa katika muda wa sekundi 55 na baadaye ndege ililipuka.Â
Maafisa wa vyombo vya dola kwa kushirikiana wanaendelea kuchunguza chanzo cha ndege hiyo kulipuka muda mfupi baada ya kutua kwa dharura katika uwanja Sheremetyvo
Taarifa za kulipuka kwa ndege hiyo tayari zimemfikia Rais wa Urusi Vladimir Putin  ameeleza masikitiko yake kwa familia za waathiriwa. Eneo hilo la Murmansk limetangaza siku tatu za maombolezi.