Mtanzania atwaa tuzo ya ubunifu nchini Misri

March 19, 2019 4:08 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  •  Rahma Bajun amepokea tuzo ya utambuzi kutoka “Arab and African Youth Platform” Jijini Aswan nchini Misri mapema jana (17 Machi 2019)

Dar es Salaam Mbunifu wa mavazi kutoka Tanzania Rahma Bajun amepokea tuzo ya utambuzi kutoka “Arab and African Youth Platform” Jijini Aswan nchini Misri mapema jana (17 Machi 2019) huku akipokea sifa lukuki kutoka kwa  Watanzania.

Mwanadada huyo, ambaye  hushiriki  kwenye  maonyesho mbalimbali, amefanikiwa kuliteka soko la mitindo ndani na nje ya nchi kwa muda mfupi huku akivalisha baadhi ya vigogo nchini wakiwamo Maria Tsehai Sarungi na Zitto Kabwe.

Saa chache baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo na Rais wa Misri Abdelfattah Elsisi pamoja na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Moussa Faki , mamia ya Watanzania walisifu kazi za mwanadada huyo kupitia kurasa za mitandao ya kijamii ikiwemo Twitter.

Baadaye kidogo, Bajun aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter akisema  “Ni heshima kwangu na kwa nembo ya MnM na kwa Tanzania kupokea tuzo hii sambamba na vijana mahiri kutoka Uarabuni na Africa.”

Kinachovutia zaidi juu ya ubunifu wake ni kwamba Rahma hutumia malighafi zinazotengenezwa nchini kwa kuwa kwa asilimia kubwa hushona mavazi yatokanayo na vitenge ama khanga.

Wengi wanamfahamu Rahma kama mbunifu wa mavazi anayechipukia nchini Tanzania lakini huenda siku zijazo neno anachipukia likabadilishana na “mwenye mafanikio zaidi” kwa kuwa amekuwa akikua siku hadi siku kupiga hatua katika kazi za ubunifu.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.