Mtanzania atwaa tuzo ya ubunifu nchini Misri

March 19, 2019 4:08 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  •  Rahma Bajun amepokea tuzo ya utambuzi kutoka “Arab and African Youth Platform” Jijini Aswan nchini Misri mapema jana (17 Machi 2019)

Dar es Salaam Mbunifu wa mavazi kutoka Tanzania Rahma Bajun amepokea tuzo ya utambuzi kutoka “Arab and African Youth Platform” Jijini Aswan nchini Misri mapema jana (17 Machi 2019) huku akipokea sifa lukuki kutoka kwa  Watanzania.

Mwanadada huyo, ambaye  hushiriki  kwenye  maonyesho mbalimbali, amefanikiwa kuliteka soko la mitindo ndani na nje ya nchi kwa muda mfupi huku akivalisha baadhi ya vigogo nchini wakiwamo Maria Tsehai Sarungi na Zitto Kabwe.

Saa chache baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo na Rais wa Misri Abdelfattah Elsisi pamoja na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Moussa Faki , mamia ya Watanzania walisifu kazi za mwanadada huyo kupitia kurasa za mitandao ya kijamii ikiwemo Twitter.

Baadaye kidogo, Bajun aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter akisema  “Ni heshima kwangu na kwa nembo ya MnM na kwa Tanzania kupokea tuzo hii sambamba na vijana mahiri kutoka Uarabuni na Africa.”

Kinachovutia zaidi juu ya ubunifu wake ni kwamba Rahma hutumia malighafi zinazotengenezwa nchini kwa kuwa kwa asilimia kubwa hushona mavazi yatokanayo na vitenge ama khanga.

Wengi wanamfahamu Rahma kama mbunifu wa mavazi anayechipukia nchini Tanzania lakini huenda siku zijazo neno anachipukia likabadilishana na “mwenye mafanikio zaidi” kwa kuwa amekuwa akikua siku hadi siku kupiga hatua katika kazi za ubunifu.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
17 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
17 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
17 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Siku ya Familia, Mtoto wa Afrika kuadhimishwa Juni 30, 2026

Siku ya Familia, Mtoto wa Afrika kuadhimishwa Juni 30, 2026

Nukta TV

Wadau wa 'kubet" watoa ya moyoni, pendekezo kupanda kwa tozo 5%

Wadau wa 'kubet" watoa ya moyoni, pendekezo kupanda kwa tozo 5%

Nukta TV

Wasemayo wananchi, vocha za kukwangua kupigwa maruku mijini

Wasemayo wananchi, vocha za kukwangua kupigwa maruku mijini

Nukta TV