Morogoro inavyokimbiza uzalishaji wa nyanya

March 18, 2020 2:42 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni baada ya kulima zaidi ya nusu ya nyanya zote Tanzania bara.
  • Morogoro imefuatiwa na mkoa wa Kilimanjaro na Mtwara.
  • Mkoa huo ulizalisha tani 155,745 sawa na asilimia 65.5 ya nyanya zote zilizozalishwa mwaka huo.

Dar es Salaam. Mkoa wa Morogoro umetajwa kuongoza kwa kilimo cha nyanya baada ya kuzalisha zaidi ya nusu ya nyanya zote Tanzania bara. 

Kwa mujibu wa ripoti ya Utafiti wa Mwaka wa Sekta ya Kilimo (AAS 2016/2017) iliyotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) mwaka 2016/2017 mkoa huo ulizalisha tani 155,745 sawa na asilimia 65.5 ya nyanya zote zilizozalishwa mwaka huo. 

Hiyo ni sawa na kusema zaidi ya nusu ya nyanya zote zinazozalishwa Tanzania zinatoka katika mkoa huo unaopatikana Mashariki mwaka Tanzania. 

Morogoro inafuatiwa kwa mbali na Kilimanjaro ambayo iliyozalisha tani 18,630 na Mtwara katika nafasi ya tatu baada ya kuzalisha tani 13,336.

Nyanya limekuwa ni zao la mboga ambalo linatumiwa zaidi katika shughuli za mapishi nyumbani na usindikaji wa bidhaa mbalimbali ikiwemo nyanya za kopo. 

Habari hii imeboreshwa kiunganishi (link) ya chanzo cha takwimu Machi 8, 2020.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.