Morogoro inavyokimbiza uzalishaji wa nyanya
- Ni baada ya kulima zaidi ya nusu ya nyanya zote Tanzania bara.
- Morogoro imefuatiwa na mkoa wa Kilimanjaro na Mtwara.
- Mkoa huo ulizalisha tani 155,745 sawa na asilimia 65.5 ya nyanya zote zilizozalishwa mwaka huo.
Dar es Salaam. Mkoa wa Morogoro umetajwa kuongoza kwa kilimo cha nyanya baada ya kuzalisha zaidi ya nusu ya nyanya zote Tanzania bara.
Kwa mujibu wa ripoti ya Utafiti wa Mwaka wa Sekta ya Kilimo (AAS 2016/2017) iliyotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) mwaka 2016/2017 mkoa huo ulizalisha tani 155,745 sawa na asilimia 65.5 ya nyanya zote zilizozalishwa mwaka huo.
Hiyo ni sawa na kusema zaidi ya nusu ya nyanya zote zinazozalishwa Tanzania zinatoka katika mkoa huo unaopatikana Mashariki mwaka Tanzania.
Morogoro inafuatiwa kwa mbali na Kilimanjaro ambayo iliyozalisha tani 18,630 na Mtwara katika nafasi ya tatu baada ya kuzalisha tani 13,336.
Nyanya limekuwa ni zao la mboga ambalo linatumiwa zaidi katika shughuli za mapishi nyumbani na usindikaji wa bidhaa mbalimbali ikiwemo nyanya za kopo. 
Habari hii imeboreshwa kiunganishi (link) ya chanzo cha takwimu Machi 8, 2020.
Latest