Miradi ya jotoardhi yashika kasi Mbeya, Songwe

September 22, 2022 3:56 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Inaendeshwa na kampuni ya Uendelezaji Jotoardhi Tanzania (TGDC).
  • Bodi mpya ya TGDC yaridhishwa na utekelezaji wake.
  • Kuzalisha megawati 200 ifikapo 2025.

Matumizi ya nishati jadidifu yanazidi kushika kasi Tanzania, baada ya kampuni ya Uendelezaji Jotoardhi Nchini (TGDC) kujipanga kuzalisha umeme wa megawati 200 unaotokana na jotoardhi ifikapo mwaka 2025.

Kwa mujibu wa TGDC, Tanzania ina uwezo wa kuzalisha umeme wa jotoardhi usiopungua megawati 5,000 katika maeneo zaidi ya 50 katika mikoa 16 nchini. 

Ili kufikia lengo la kuzalisha umeme wa jotoardhi wa megawati 200, TGDC inatekeleza miradi mitano ya kipaumbele ambayo ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji. 

Miradi hiyo ni Ngozi megawati 70 na Kiejo-Mbaka (megawati 60) iliyopo Mbeya, Songwe (megawati 5) mkoani Songwe, Luhoi (megawati 5) Pwani, na Natron megawati 60 mkoani Arusha.

Bodi ya TGDC yaridhishwa na kazi

Licha ya TGDC kuendelea na miradi yake mitano ya jotoardhi, imekuwa ikifuatiliwa kwa karibu kuhakikisha inatekelezwa kama ilivyopangwa ili kuwanufaisha Watanzania na Taifa hasa kuwapatia nishati endelevu na rafiki kwa mazingira. 

Bodi ya TGDC imefanya ziara ya siku tatu kutembelea miradi ya kimkakati inayotekelezwa na kampuni hiyo mikoani Mbeya na Songwe akiambatana na uongozi wa kampuni hiyo ili kujionea utekelezaji wake.

Ziara hiyo ambayo ni ya kwanza tangu bodi hiyo ilipozinduliwa Julai 2022,  iliongozwa na Mwenyekiti wake Profesa Shubi Kaijage ambaye ameridhishwa na maendeleo ya utekelezaji wa miradi hiyo ya TGDC, kampuni tanzu hii ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco).

“Tumefarijika na maendeleo na jitihada zinazoendelea katika miradi ya jotoardhi, na tunaendelea kuishauri na kuielekeza Menejimenti ya TGDC ili tufikie malengo ya megawati 200 ifikapo mwaka 2025 kama mipango mikakati ya kampuni ilivyoainishwa  na kutimiza malengo ya Serikali yetu,” amesema Prof Kaijage. 

Nishati ya jotoardhi ina matumizi mengi ikiwemo kuzalisha umeme ambao hutumika kuendeshea mitambo, kupikia na kutoa mwanga majumbani.

Kwa mujibu Kaimu Meneja Mkuu wa TGDC Mhandisi Shakiru Idrissa, kazi ya kuchoronga visima vya jotoardhi itafanyika kwa kipindi cha miezi minne hadi sita kwa upande wa mradi wa Ngozi baada ya kuwasili kwa mtambo mwishoni mwa Oktoba. 

“Kampuni inategemea kupata Megawati 70 za awali kwa vipindi vya awamu mbili, awamu ya kwanza megati 30 na ya pili megawati 40 ifikapo mwaka 2025 (kwa mradi wa Ngozi),” amesema Mhandisi Idrissa.

Katika ziara hiyo Bodi ya Wakurugenzi ya TGDC ilifika katika mradi wa Kiejo-Mbaka uliopo Mbeya, ambapo TGDC imeishachoronga visima vifupi vitatu vya utafiti ambapo megawati 60 zinatarajiwa kuzalishwa.

Katika mradi wa Songwe, umeme wa jotoardhi wa megawati 5 hadi 38 unaratajiwa kuzalishwa.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV