Mhadhiri UDSM ateuliwa kuwa mwenyekiti bodi ya NBS
September 25, 2019 11:16 am ·
Rodgers Raphael
- Rais John Magufuli amemteua Dk Amina Msengwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) akichukua nafasi ya mtangulizi wake, Adrew Masawe.
- Dk Msengwa alikuwa Mhadhiri na Mkuu wa Idara ya Takwimu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Dar es Salaam. Rais John Magufuli amemteua Dk Amina Msengwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) akichukua nafasi ya mtangulizi wake, Adrew Masawe.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu iliyotolewa leo (Septemba 25, 2019), uteuzi huo umefanyika baada ya Masawe kumaliza muda wake katika kuitumikia bodi hiyo.
Kabla ya uteuzi huo, Dk Msengwa alikuwa Mhadhiri na Mkuu wa Idara ya Takwimu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
U T E U Z I. pic.twitter.com/uia4RoNM5h
— Gerson Msigwa (@MsigwaGerson) September 25, 2019
Latest
5 days ago
·
Lucy Samson
Vita ya Mashariki ya Kati yazidi kupaisha bei ya petroli, dizeli Tanzania
6 days ago
·
Kelvin Makwinya
Viwango vya kubadili fedha Machi 31, 2026
7 days ago
·
Lucy Samson
ATCL yaripoti hasara ya Sh191.1 bilioni, CAG aanika sababu
7 days ago
·
Kelvin Makwinya
Rais Samia apokea ripoti CAG, TAKUKURU na PPRA aagiza utekelezaji wa haraka