Mchengerwa aipa Wizara ya Afya mwelekeo mpya, watumishi waonywa

December 8, 2025 5:49 pm · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link
  • Aagiza kuanza kwa mchakato wa ithibati ya kimataifa na matumizi ya teknolojia za kisasa sekta ya afya.
  • Watumishi wa afya waonywa kutokana na ucheleweshaji wa huduma kwa wagonjwa.

Dar es Salaam. Waziri wa Afya Mohamed Mchengerwa amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dk Seif Shekalaghe, kuhakikisha hospitali zote za kanda zinaanza mara moja mchakato wa kupata Ithibati ya kimataifa ili kuongeza ubora na kutambulika kimataifa.

Waziri Mchengerwa aliyekuwa akizungumza leo Desemba 8, 2025 kwenye kikao kazi na watumishi wa sekta ya afya jijini Dar es Salaam kilichofanyika katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Upanga, amesema kuwa ithibati hizo zitaziwezesha taasisi za afya nchini kuendana na viwango vya kimataifa, hatua itakayoboresha utoaji wa huduma pamoja na kuongeza pato la Taifa. 

“Ninazielekeza hospitali zote za kanda, taasisi zetu zote kuanza mchakato wa kupata ithibati za kimataifa. Tutakuwa na vigezo mahsusi ambavyo tutalazimika kuvifuata. Tutaongeza utolewaji wa huduma lakini pia kuongeza pato la Taifa kwa kupata wageni kutoka maeneo mbalimbali,” ameeleza Waziri Mchengerwa.

Pamoja na agizo hilo, Mchengerwa amemtaka Katibu Mkuu kusimamia uanzishwaji wa viwanda vya dawa na vifaa tiba, kuimarisha ‘medical tourism’ (Tiba utalii) kama chanzo kipya cha mapato na kuimarisha huduma za afya ya kinga.

Vile vile, kuongeza nguvu katika utafiti, ubunifu na tiba shirikishi, pamoja na kuhakikisha matumizi ya teknolojia za kisasa ikiwemo mifumo ya afya ya kidijitali na akili unde (digital health na AI) yanaimarishwa katika mfumo wa afya.

Katika hatua nyingine, Waziri Mchengerwa ametoa wito kwa viongozi na watumishi wa sekta ya afya nchini kuhakikisha wagonjwa wanahudumiwa kwa wakati ili kuondoa foleni zisizo za lazima.

Aidha, amesema foleni mara nyingi si matokeo ya wingi wa wagonjwa bali ni dalili ya udhaifu wa mifumo ya utoaji huduma, akiwataka watumishi kuchukua hatua za kuboresha mifumo hiyo mara moja.

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dk. Delilah Kimambo, amesema hospitali hiyo inatekeleza majukumu yake kupitia Kurugenzi 14, Idara 54 na Vitengo 228. 

Watumishi Sekta ya afya waonywa

Waziri Mchengerwa ametoa onyo kali kwa viongozi wa taasisi na watumishi wa sekta ya afya, akiwataka kubadilika na kuwahudumia wagonjwa kwa weledi na kwa wakati.

Amesema haikubaliki wagonjwa kusubiri huduma kwa muda mrefu kwa sababu ya changamoto ambazo zinaweza kutatuliwa mara moja katika mazingira ya kawaida.

Akitolea mfano, Mchengerwa amesema Taasisi ya Saratani ya Ocean Road imepokea mashine mpya ya matibabu lakini haijaanza kutumika kwa madai ya kusubiri hafla ya ufunguzi.

Aidha, ameeleza kuwa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) ina mashine tatu ambazo hazifanyi kazi kwa takribani miezi miwili, bila hatua madhubuti kuchukuliwa, hali inayosababisha wagonjwa kukosa huduma muhimu.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV