Mavazi ya wanawake yachangia kupaisha mfumuko wa bei Tanzania

July 9, 2021 6:22 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Umepanda hadi kufikia asilimia 3.6 kwa mwaka ulioishia mwezi Juni, 2021 kutoka asilimia 3.3 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei, 2021.
  • Umechangiwa na kuongezeka kwa bei ya baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula vikiwemo vitambaa vya nguo na mavazi ya wanawake.

Dar es Salaam. Kasi ya mfumuko wa bei za bidhaa na huduma nchini imepanda hadi kufikia asilimia 3.6 kwa mwaka ulioishia mwezi Juni, 2021 kutoka asilimia 3.3 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei, 2021.

Kasi hiyo imechangiwa na kuongezeka kwa bei ya baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula vikiwemo vitambaa vya nguo na mavazi ya wanawake.

Mfumuko wa bei wa Taifa hupima kiwango cha kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma zote zinazotumiwa na kaya binafsi nchini.

Kwa mujibu wa taarifa ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) iliyotolewa Julai 8, 2021, bei ya vitambaa vya nguo imepanda kwa asilimia 8.5, nguo za wanawake (asilimia 6.3), viatu vya wanaume kwa asilimia 6.2. 

Kodi ya pango kwa asilimia 4.9, vyakula kwenye migahawa (asilimia 5.6) na gharama za malazi kwenye nyumba za kulala wageni zimepanda kwa asilimia 5.7..

Mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwaka ulioishia mwezi Juni, 2021 umepungua hadi asilimia 4.7 kutoka kwa asilimia 4.9 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei, 2021.

Hali ya mfumuko wa bei Afrika Mashariki

Nchini Kenya, mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Juni, 2021 umeongezeka hadi asilimia 6.4 kutoka asilimia 5.8 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei, 2021. 

Kwa upande wa Uganda, mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia mwezi Juni, 2021 umeongezeka pia hadi asilimia 2 kutoka asilimia 1.9 kwa mwaka ulioishia mwezi Mei, 2021.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
6 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
6 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV