Maumivu: Bei za mafuta zapaa

March 8, 2018 6:07 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Watumiaji kutoka mikoa ya Kaskazini mwa nchi wao hawataguswa na maumivu ya bei mpya za mafuta kwa kuwa Bandari ya Tanga haikuingiza shehena mpya ya nishati hiyo.

Dar es Salaam. Watumiaji wa mafuta nchini watalazimika kutoboa mifuko yao zaidi baada ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) kutangaza bei mpya za rejareja za nishati hiyo ambazo mwezi huu zimepaa ikilinganishwa na Februari kutokana na mabadiliko katika soko la dunia, kuongezeka kwa gharama za usafirishaji wa mafuta na kushuka kwa thamani ya Shilingi dhidi ya Dola ya Marekani.

Hata hivyo, maumivu hayo hayatawagusa wakazi wa mikoa ya Kaskazini kwa kuwa bei za mafuta hazijabadilika kwa kuwa Bandari ya Tanga haikuingiza mzigo mpya mwezi uliopita.

Katika bei hizo mpya, Ewura inaeleza kuwa watumiaji wa Dizeli watalipa Sh69 zaidi kwa lita ikilinganishwa na ilivyokuwa Februari wakati wale wa Petroli watatakiwa kuongeza Sh1 kwa lita. Watumiaji wa Mafuta ya Taa wao watalipa Sh4 kwa lita zaidi ya ilivyokuwa Februari. 


Soma zaidi: Shule 24 vigogo ‘zilizoteka’ 10 bora kidato cha nne


“Ifahamike kwamba katika shehena sita za mafuta zilizopokelewa katika Bandari ya Dar es Salaam katika mwezi Februari, tano zilinunuliwa kwa bei ya soko la dunia za Disemba 2017 na moja ilinunuliwa kwa bei ya soko la dunia ya mwezi Januari 2018,” inasomeka sehemu ya taarifa ya Ewura iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Nzinyangwa Mchany. 

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.