Maumivu: Bei za mafuta zapaa

March 8, 2018 6:07 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Watumiaji kutoka mikoa ya Kaskazini mwa nchi wao hawataguswa na maumivu ya bei mpya za mafuta kwa kuwa Bandari ya Tanga haikuingiza shehena mpya ya nishati hiyo.

Dar es Salaam. Watumiaji wa mafuta nchini watalazimika kutoboa mifuko yao zaidi baada ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) kutangaza bei mpya za rejareja za nishati hiyo ambazo mwezi huu zimepaa ikilinganishwa na Februari kutokana na mabadiliko katika soko la dunia, kuongezeka kwa gharama za usafirishaji wa mafuta na kushuka kwa thamani ya Shilingi dhidi ya Dola ya Marekani.

Hata hivyo, maumivu hayo hayatawagusa wakazi wa mikoa ya Kaskazini kwa kuwa bei za mafuta hazijabadilika kwa kuwa Bandari ya Tanga haikuingiza mzigo mpya mwezi uliopita.

Katika bei hizo mpya, Ewura inaeleza kuwa watumiaji wa Dizeli watalipa Sh69 zaidi kwa lita ikilinganishwa na ilivyokuwa Februari wakati wale wa Petroli watatakiwa kuongeza Sh1 kwa lita. Watumiaji wa Mafuta ya Taa wao watalipa Sh4 kwa lita zaidi ya ilivyokuwa Februari. 


Soma zaidi: Shule 24 vigogo ‘zilizoteka’ 10 bora kidato cha nne


“Ifahamike kwamba katika shehena sita za mafuta zilizopokelewa katika Bandari ya Dar es Salaam katika mwezi Februari, tano zilinunuliwa kwa bei ya soko la dunia za Disemba 2017 na moja ilinunuliwa kwa bei ya soko la dunia ya mwezi Januari 2018,” inasomeka sehemu ya taarifa ya Ewura iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Nzinyangwa Mchany. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
19 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
19 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
19 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Siku ya Familia, Mtoto wa Afrika kuadhimishwa Juni 30, 2026

Siku ya Familia, Mtoto wa Afrika kuadhimishwa Juni 30, 2026

Nukta TV

Wadau wa 'kubet" watoa ya moyoni, pendekezo kupanda kwa tozo 5%

Wadau wa 'kubet" watoa ya moyoni, pendekezo kupanda kwa tozo 5%

Nukta TV

Wasemayo wananchi, vocha za kukwangua kupigwa maruku mijini

Wasemayo wananchi, vocha za kukwangua kupigwa maruku mijini

Nukta TV