Matumizi ya SMS yapungua kwa asilimia 3 Tanzania

October 25, 2024 5:09 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Yafikia bilioni 47.6 kutoka bilioni 50.8 iliyorekodiwa kipindi cha robo ya mwaka inayoishia Juni, 2024.

Arusha. Huenda ongezeko la nyanja za mawasiliano  na majukwa ya huduma za ujumbe wa papo hapo kama WhatsApp, Facebook Messenger, na Telegram yakaathiri njia za mawasiliano za zamani ikiwemo ujumbe mfupi (SMS) mara baada ya takwimu kuripoti kupungua kwa matumizi ya sms kwa asilimia tatu.

Kwa muda mrefu Watanzania hususan wenye simu za mkononi maarufu kama simu za vitochi wamekuwa wakitumia SMS kuwasiliana na wapendwa wao lakini huenda desturi hiyo ikabadilika hivi karibuni.

Idadi ya SMS inayozungumziwa ni zile zilizotumwa  ndani na nje ya mtandao kuanzia mwezi Julai hadi Septemba kupitia mitandao ya Artel, TTCL, Tigo, Vodacom na Halotel.

Takwimu za mawasiliano za  robo ya mwaka unaoishia Septemba 2024 zinazotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) zinabainisha kuwa idadi ya ujumbe mfupi wa maneno uliotumwa ndani ya nchi ni bilioni 47.6.

Kati ya hizo SMS zilitumwa ndani ya mtandao ni blioni 20.2 na nje ya mtandao bilioni 27.4.

Katika kipindi cha robo ya mwaka inayoishia Juni, 2024. Jumla ya SMS 50.8 bilioni zilirekodiwa ikijumlisha SMS 25.1 za ndani na 29.3 za nje.

Huenda kupungua kwa matumizi hayo kumechagizwa na kuongezeka kwa matumizi ya mawasiliano kwa njia ya mtandao yanayowezeshwa na matumizi ya intaneti ambayo TCRA imeripoti kuongezeka.

Kwa mujibu wa TCRA Idadi ya laini za Intaneti imeongezeka kwa asilimia 5 kutoka milioni 39.3 kwa robo ya mwaka iliyoishia Juni 2024 hadi milioni 41.4 kwa robo ya mwaka iliyoishia Septemba 2024.

Matumizi hayo ya intaneti hupimwa kwa kuangalia  laini ambazo zimetumia huduma ya Intaneti angalau mara moja katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita, bila kujali teknolojia iliyotumika.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
9 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
9 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Ulinzi waimarishwa Dar, maduka yachelewa kufunguliwa

Ulinzi waimarishwa Dar, maduka yachelewa kufunguliwa

Nukta TV

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV