Mambo ya kufanya unapohisi gesi imevuja nyumbani

August 5, 2022 8:59 am · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link
  • Fungua madirisha na milango kuruhusu hewa kuingia ndani.
  • Usiwashe taa au friji unapohisi gesi inavuja.

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetoa tahadhari zinazopaswa kuchukuliwa kwa mtumiaji wa gesi ya majumbani (LPG) pale wanapohisi inavuja ikiwemo kufungua madirisha na milango kuruhusu hewa iingie ndani.

Akizungumza Nukta habari (www.nukta.co.tz) kwenye maonyesho ya Nane Nane yanayofanyika nje kidogo ya jiji la Mwanza katika viwanja vya Nyamhongolo, Meneja wa Ewura Kanda ya Ziwa, George Mhina amesema pamoja na kwamba Serikali inahamasisha matumizi ya nishati hiyo ya kupikia lakini watumiaji wanapaswa kuwa waangalifu pale wanapohisi kuna kihitarishi kinachosababishwa na gesi hiyo.

Mhina ameainisha mambo muhimu manne yanayopaswa kuzingatiwa iwapo mtumiaji atahisi kuna harufu ya gesi au gesi inavuja ndani ya nyumba yake. Mojawapo ni kutowasha taa kwa kuwa zipo taa ambazo zinaweza kusababisha cheche na kusababisha mlipuko.

Pia mtumiaji hapaswi kufungua jokofu au friji, asiwashe kiberiti na anatakiwa kufungua madirisha ili kuruhusu hewa safi kuingia nadani ya nyumba.

“ Tunaendelea kutoa elimu hii kwa kuwa hivi sasa Serikali imeanza kuhamasisha matumizi ya gesi hadi vijijini, hivyo ili kuepuka matatizo yanayoweza kusababishwa na gesi kuvuja  jamii inatakiwa kujua mbinu hizo muhimu,” amesema Mhina. 

Meneja huyo pia ametumia fursa hiyo kuwataka wauzaji wa mitungi ya gesi kuacha uchakachuaji wa gesi na atakayebainika atachukuliwa hatua za kisheria.

Mhina amewataka watumiaji pale wanapoenda kununua gesi kuhakikisha wanaipima ili kuona ujazo wa gesi kama uko sawa kulingana na kiwango alichoenda kununua lakini pia kuangalia lakiri.

“Pia tunawaasa watumiaji wanaposafirisha gesi wahakikishe wanaiacha angalau kwa muda wa dakika tano ndipo aanze kuitumia,” amesema Mhina.

Hata hivyo amesema hivi sasa Serikali inapambana kuhakikisha wananchi wanatumia nishati mbadala ili kupunguza matumizi ya kuni na mkaa.

Anasema mbali na uharibifu wa mazingira lakini pia nishati hiyo ya kuni na mkaa inasababisha magonjwa ya ngozi na macho na wakati mwingine akina mama kuitwa wachawi.

“Kiuhalisia mtu anayetumia kilo sita za mkaa kwa siku angetumia gesi angetumia kilo moja hivyo badala ya kutumia Sh2,000 kununulia mkaa na kuni kila siku angenunua gesi angeweza kutumia kilo sita tu kwa mwezi,” amesema Mhina.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV