Majaliwa: Njooni muwekeze Tanzania

October 26, 2022 12:24 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Awaomba wawekezaji wa Korea Kusini kujenga viwanda vya dawa nchini. 

Dar es Salaam. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kutokana na mpango wa Serikali wa kuendelea kuimarisha eneo la utoaji huduma za afya, Tanzania inawakaribisha wawekezaji kutoka Korea Kusini kwa ajili ya kujenga viwanda vya dawa na vifaa tiba ili kuwezesha upatikanaji rahisi wa dawa na vifaa tiba. 

               

Majaliwa ametoa kauli hiyo leo Oktoba 26, 2022 baada ya kushuhudia utiaji saini wa Makubaliano ya Ushirikiano baina ya Bohari ya Dawa Tanzania (MSD) na Serikali ya Jimbo la Chungcheongbuck nchini Korea kusini.

Sehemu ya makubaliano katika mkataba huo ni kujadili na kuendeleza mahusiano ya kibiashara katika nyanja za masoko ya bidhaa zinazozalishwa na Makampuni ya dawa katika jimbo hilo.

Maeneo mengine ni kubadilishana watumishi, semina za pamoja za wataalamu wao katika nyanja mbalimbali, kubadilishana na kupeana taarifa za uwekezaji kwenye sekta ya dawa, msaada wa kitaalamu na wataalam.

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW