Magufuli atoa maagizo mazito uvunaji mamba, viboko

October 7, 2019 1:20 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Asema wanatakiwa kuvunwa kisayansi ili wasimalizwe wote.
  • Awataka wananchi wasiwafuate kwenye maziwa na mito.

Dar es Salaam. Rais John Magufuli ameitaka Wizara ya Maliasili na Utalii kuangalia namna nzuri ya kuvuna mamba na viboko kwa njia ya kisayansi na kuwaelimisha wananchi juu ya matumizi sahihi ya mito na maziwa ili kupunguza vifo, uharibifu wa mazao na makazi.

Dk Magufuli aliyekuwa akizungumza leo (Oktoba 7, 2019) mkoani Rukwa, amesema wizara ihusike katika kupanga mikakati ni kwa namna gani wanaweza kuanza mipango ya kuwavuna mamba na viboko na kuwatumia kama vitoweo ili kuwapunguza katika vyanzo vya maji.

“Hawa wanyama tuliopewa na Mungu ni lazima watusaidie katika kujenga uchumi wetu lakini pia wasimalizwe ni lazima uvunaji (wa mamba na viboko) uwe wa kisayansi kwa manufaa ya wote,” amesema Magufuli. 

Pamoja na hayo, Rais ameutaka uongozi wa Mkoa wa Rukwa na wizara inayohusika na wanyama pori waelemishwe na wajue madhara ya kusogea kwenye mito na maziwa hasa ziwa Rukwa.  

“Kwa hiyo ni lazima wote tujipange katika kushare (kutumia pamoja) ardhi tuliyopewa na Mungu. Wananchi wasisogee sana kujenga makazi yao na kulima mazao  kando kando ya Ziwa Rukwa, ambavyo kwa vyovyote viboko watakuja kuyala,” amesema Rais. 


Soma zaidi: 


Agosti 17, 2019, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla alisema Serikali itauza asilimia 10 ya mamba wote nchini ikiwa ni hatua ya kukabiliana na ongezeko la wanyama wakali na wanaovamia maeneo ya watu na kufanya uharibifu ikiwemo kusababisha vifo. 

Aidha, Kigwangalla alisema watauza viboko wote waliopo kwenye maeneo yenye maji kama maziwa, mabwawa na mito iliyopo mjini ukiwemo mji wa Mpanda mkoani Katavi, Mafia (Pwani) na Babati (Manyara).

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV