Magufuli asaini sheria nne zilizopitishwa bungeni
- Sheria hizo ni pamoja na Sheria ya Serikali Mtandao namba 10 ya mwaka 2019.
- Zilipitishwa katika katika mkutano wa 16 wa Bunge la Tanzania Septemba mwaka huu.
- Sheria zilizosainiwa zimetangazwa kwenye gazeti la Serikali na zitapatikana kwenye tovuti ya Bunge.
Dar es Salaam. Rais John Magufuli amesaini sheria nne ikiwemo ya Sheria ya Serikali Mtandao namba 10 ya mwaka 2019 zilizopitishwa katika mkutano wa 16 wa Bunge la Tanzania ili zianze kutumika rasmi.
Mkutano huo uliofanyika Septemba mwaka huu pamoja na mambo mengine ulipitisha sheria hizo ili zitumike katika shughuli mbalimbali za utawala.
Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Bunge leo (Octoba 1 2019)inaeleza kuwa sheria hizo zilizosainiwa na Rais, zimetangazwa katika gazeti la Serikali.
Sheria hizo ni pamoja na Sheria ya Serikali Mtandao Na. 10 ya mwaka 2019 ambayo inalenga kusimamia kuwepo kwa uthabiti wa kisheria utakaozuia urudufu wa mifumo na miundombinu ya Serikali mtandaoni.
Zinazohusiana
Nyingine ni Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 4), Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 5) pamoja na Sheria ya marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 6) zote za mwaka 2019.
Sheria Nne zilizopitisha katika Mkutano wa 16 wa Bunge zimeshasainiwa na Mheshimiwa Rais na kutangazwa katika Gazeti la Serikali.Sheria hizo pia zinapatikana kwenye Tovuti ya Bunge ambayo ni https://t.co/YLJSmCtyiP
pic.twitter.com/ovBVhvrVrC— Bunge la Tanzania (@bunge_tz) October 1, 2019
Latest