Magufuli asaini sheria nne zilizopitishwa bungeni

October 1, 2019 7:57 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Sheria hizo ni pamoja na Sheria ya Serikali Mtandao namba 10 ya mwaka 2019.
  • Zilipitishwa katika katika mkutano wa 16 wa Bunge la Tanzania Septemba mwaka huu. 
  • Sheria zilizosainiwa zimetangazwa kwenye gazeti la Serikali na zitapatikana kwenye tovuti ya Bunge.

Dar es Salaam. Rais John Magufuli amesaini sheria nne ikiwemo ya  Sheria ya Serikali Mtandao namba 10 ya mwaka 2019 zilizopitishwa katika mkutano wa 16 wa Bunge la Tanzania  ili zianze kutumika rasmi.

Mkutano huo uliofanyika Septemba mwaka huu pamoja na mambo mengine ulipitisha sheria hizo ili zitumike katika shughuli mbalimbali za utawala. 

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Bunge leo (Octoba 1 2019)inaeleza kuwa sheria hizo zilizosainiwa na Rais, zimetangazwa katika gazeti la Serikali.

Sheria hizo ni pamoja na Sheria ya Serikali Mtandao Na. 10 ya mwaka 2019 ambayo inalenga kusimamia kuwepo kwa uthabiti wa kisheria utakaozuia urudufu wa mifumo na miundombinu ya Serikali mtandaoni.


Zinazohusiana


Nyingine ni Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 4), Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 5) pamoja na Sheria ya marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 6) zote za mwaka 2019.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV