Magufuli asaini sheria nne zilizopitishwa bungeni

October 1, 2019 7:57 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Sheria hizo ni pamoja na Sheria ya Serikali Mtandao namba 10 ya mwaka 2019.
  • Zilipitishwa katika katika mkutano wa 16 wa Bunge la Tanzania Septemba mwaka huu. 
  • Sheria zilizosainiwa zimetangazwa kwenye gazeti la Serikali na zitapatikana kwenye tovuti ya Bunge.

Dar es Salaam. Rais John Magufuli amesaini sheria nne ikiwemo ya  Sheria ya Serikali Mtandao namba 10 ya mwaka 2019 zilizopitishwa katika mkutano wa 16 wa Bunge la Tanzania  ili zianze kutumika rasmi.

Mkutano huo uliofanyika Septemba mwaka huu pamoja na mambo mengine ulipitisha sheria hizo ili zitumike katika shughuli mbalimbali za utawala. 

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Bunge leo (Octoba 1 2019)inaeleza kuwa sheria hizo zilizosainiwa na Rais, zimetangazwa katika gazeti la Serikali.

Sheria hizo ni pamoja na Sheria ya Serikali Mtandao Na. 10 ya mwaka 2019 ambayo inalenga kusimamia kuwepo kwa uthabiti wa kisheria utakaozuia urudufu wa mifumo na miundombinu ya Serikali mtandaoni.


Zinazohusiana


Nyingine ni Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 4), Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 5) pamoja na Sheria ya marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na. 6) zote za mwaka 2019.

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW