Kutana na majiko banifu yanayotumia umeme

August 31, 2022 3:48 pm · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link
  • Yanatumia kiasi kidogo cha umeme
  • Ni rafiki wa mazingira na afya za watu.
  • Yana uwezo wa kupika vyakula vya aina mbalimbali.

Kama wewe ni miongoni mwa watu wanaomini kupikia chakula kwenye majiko ya umeme ni gharama, fahamu kuwa unahitaji elimu zaidi.

Nishati hiyo umeme ni rahisi na ya haraka kupikia, rafiki wa mazingira na afya ya mtumiaji. 

Majiko hayo hayatumii umeme mwingi tofauti na fikra za baadhi ya watu. Umeme kutumika mwingi inategemea na chakula unachopika au muda unaotumia jikoni.

Baadhi ya wabunifu wamebuni majiko banifu yanayotumia kiasi kidogo cha umeme, wakati huo kukidhi mahitaji ya mtumiaji. Baadhi ya majiko hayo ni yale yanayosambazwa na kampuni ya Jiko Chanya Ltd iliyopo mkoani Mwanza.

Kwa mjibu wa wakala wa majiko hayo, Doricus Nikolaus, majiko hayo hayatengenezwi nchini isipokuwa wanaagiza nje ya nchi.

Ametaja moja ya sifa ya jiko hilo kuwa halitumii umeme mwingi na unaweza kutumia umeme wa uniti 0.5 hadi 1 unaweza kupikia kwa saa moja kwa sababu “ jiko hili ni amara na salama.”

“Ni salama kwasababu hata mtoto anaweza kulitumia kwa sababu kama hujabandika sufuria jikoni jiko hilo litaendelea kuwa la baridi kabisa, joto litashika pale tu utakapobandika sufuria ya kupikia na baada ya kumaliza kupika linarudi kwenye ubaridi kawaida,” amesema Doricus.

Jiko hilo kwa kutumia sufuria maalum unaweza kuchoma nyama, kukaa chipsi bila kuweka mafuta na vyakula vingine vyote ambavyo unaweza kupikia kwenye nishati nyingine.

“Kwa kutumia jiko hili tunaweza kusababisha kupunguza matumizi ya kuni na mkaa na hivyo kutunza mazingira,” anasema Doricus.

Doricus yupo kwenye maonyesho ya wafanyabiashara ya Afrika Mashariki yanayoandaliwa Chemba ya Wafanya Biashara, Wenye Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA) ambayo hufanyika kila mwaka jijini Mwanza.

“Majiko haya yanaweza kutumia umeme kidogo mfano umeme wa Sh500 unaweza ukautumia kwa muda wa saa moja na nusu na kufanikiwa kuchemsha maharagwe ambayo ungetumia nishati nyingine ama majiko ya kawaida usingetosha” anasema Doricus mwenye uzoefu wa miaka miwili katika kazi ya kuuza majiko banifu.

Mwitiko wa ununuaji wa majiko hayo ni mkubwa kwa wakazi wa Mkoa wa Mwanza huku akiwashauri baadhi ya Watanzania kuyachangamkia ili kuwa sehemu ya kutunza mazingira.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV