Kuku wa kupaka: Mahitaji na namna ya kuandaa

May 30, 2022 12:12 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Unahitaji vipande vya kuku, kitunguu maji, kitunguu saumu, tangawizi, pilipili manga kijiko, korosho, samli na maziwa.  

Nyama ya kuku ina mapishi mbalimbali kulingana na mahitaji ya mlaji. Nyama hii ni tamu na ukiipika unavyotaka inakuwa bomba. 

Umaarufu wa kuku pia unachangiwa na wataalamu wa afya kupendekeza ulaji wa nyama nyeupe yaani ya kuku, samaki na nyama ya sungura.

Tusonge mbele. Leo jikoni tunaenda kujifunza namna ya kuandaa kuku wa kupaka au kwa lugha ya kimombo “creamy garlic chicken” ambaye unaweza kula na ugali, tambi au hata chipsi na bado ukafurahia pishi hili.

Kwa kawaida kuku mzima anatakiwa kuliwa na watu wanne ila kibongo bongo hata watu nane wanaweza kugawana vipande ili mradi tu mlo wa wakati huo upite.

Andaa kuku wako kwa kumuosha na kumkata vipande vya saizi unayotaka, kisha weka kitunguu saumu, tangawizi na ndimu. Iache nyama yako kwa dakika 20 au zaidi kabla ya kuanza kupika (marination).

Baada ya hapo anza kwa kuwasha jiko lako la gesi au umeme na injika sufuria kisha weka samli kidogo au mafuta na ukaange kuku wako kwa moto wa wastani mpaka awe na rangi ya kahawia (asiive sana)

Kisha kaanga kitunguu maji, ongeza na kitunguu saumu a tangawizi iliyosagwa kiasi cha kijiko kidogo cha chakula.

Kwenye sufuria nyingine chemsha maziwa kiasi ili kutengeneza cream (malai) utakayoitumia kuongeza uzito kwenye rosti ya kuku wako.

Weka vipande vya kuku na cream ya maziwa uliyoiandaa,  kwenye sufuria uliyokaangia vitunguu huku ukiendelea kupika kwa moto mdogo, weka punje kadhaa za kitunguu saumu na korosho kiasi, kama unapendelea.

Weka chumvi ili kuleta ladha kwenye mboga kisha angalia kama rosti lako lina uzito wa kutosha kama bado unaweza kuongeza cream ya maziwa kiasi.

Koroga na acha rosti lako lichemke, kuku akishaiva vizuri basi rosti ya kuku wa kupaka itakuwa tayari kwa kuliwa. Furahia chakula chako na uwapendao.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa wananchi kupima afya, kuacha uoga

Rais Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa wananchi kupima afya, kuacha uoga

Nukta TV

Uwepo wa vifaa, madaktari uendane na huduma inayotakiwa

Uwepo wa vifaa, madaktari uendane na huduma inayotakiwa

Nukta TV

Rais Samia: Maradhi ya moyo, saratani kwa watoto yaongezeka Tanzania

Rais Samia: Maradhi ya moyo, saratani kwa watoto yaongezeka Tanzania

Nukta TV