Kamwelwe: Serikali haijasitisha ujenzi wa bandari ya Bagamoyo

May 13, 2019 3:04 pm · Nuzulack Dausen
Share
Tweet
Copy Link

Ujenzi wa mradi huo umekuwa ukipigwa kalenda mwaka hadi mwaka kutokana na kuendelea kwa majadiliano na wawekezaji. Picha|Mtandao.


  • Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe amesema mradi huo haujasitishwa bali majadiliano yanaendelea na wawekezaji.
  • Amesema ni kweli majadiliano yamechelewa kutokana na kuwepo masharti ambayo hayana manufaa kwa upande wa Tanzania.

Dar es Salaam. Baada ya kuwepo mjadala mzito bungeni juu ya hatma ya Bandari ya Bagamoyo, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe amesema mradi huo haujasitishwa na majadiliano yanaendelea na wawekezaji baada ya “kuwepo masharti yasiyokuwa na maslahi kwa Taifa”.

Akijibu hoja za wabunge wakati akihitimisha mjadala wa bajeti ya wizara yake, Kamwelwe amesema hadi sasa Serikali inaendelea na mazungumzo na wawekezaji wa mradi huo unaotarajia kugharimu Dola za Marekani bilioni 10 sawa na Sh22.3 trilioni.

“Kuna baadhi ya wabunge walisema Serikali imekataa kuendelea na mradi sina taarifa hiyo…majadiliano yanaendelea ila ni kweli yamechelewa kutokana na kuwepo masharti ambayo hayana manufaa kwa upande wa Tanzania,” amesema waziri huyo bila kuanisha masharti hayo.

“Pale itakapofikia ukomo wa majadiliano, Serikali itatoa taarifa kwa Bunge ili na wabunge nao watoe mchango wao,” ameongeza wakati akiomba wabunge wapitishe bajeti ya wizara hiyo ya takriban Sh5 trilioni.


Soma zaidi: Bunge lahoji kutojenga bandari ya Bagamoyo


Ujenzi wa mradi huo umekuwa ukipigwa kalenda mwaka hadi mwaka kutokana na kuendelea kwa majadiliano na wawekezaji.

Mwishoni mwaka 2017 Serikali ilieeleza kuwa ujenzi wa mradi huenda ungeanza Januari 2018 na kukamilika 2022 lakini hadi sasa bado haujaanza.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.