Kama ni supu basi ya utumbo ndiyo yenyewe

July 25, 2022 3:44 pm · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link
  • Supu hii ni maarufu kwa watu wengi.
  • Andaa utumbo wako wa mbuzi au ng’ombe kilo moja, kitunguu na tangawizi iliyosagwa. 

Mwanza. Nyama ya utumbo ni kipande cha nyama inayotoka katika tumbo la wanyama kama vile ng’ombe, nguruwe, kondoo au mbuzi.

Tamaduni nyingi kote ulimwenguni zimekuwa zikitumia utumbo kwa muda mrefu kama chanzo cha protini watu. Hata kwenye migahawa hupendelea kuomba supu ya utumbo na chapati kama kitafunio.

Pamoja na faida hizo leo tunataka kuangalia namna supu hii ya utumbo inavyoandaliwa.

Andaa utumbo wako wa mbuzi au ng’ombe kilo moja, kitunguu saumu kilichosagwa robo kijiko cha chai na tangawizi iliyosagwa nusu kijiko cha chai.

Tuingie jikoni

Osha utumbo vizuri kisha katakata katika vipande vidogo kulingana na saizi unayotaka. Weka utumbo kwenye sufuria, weka limao, chumvi, kitunguu swaumu, tangawizi koroga vichanganyike vizuri.

Viungo husaidia supu kuwa na harufu na ladha nzuri. Baada ya hapo bandika sufuria lako jikoni na uweke maji ya kutosha. Funika na uuache uive vizuri. Ikiwa tayari ipua na anza kula unaweza kutafunia kwa chapati au mandazi.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV