Jinsi ya kutengeneza juisi ya ukwaju

November 3, 2022 3:01 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Inafaa sana  kutumiwa kipindi cha jua kali.
  • Ina wingi wa Vitamini B, C na  K.
  • Inafaa kwa ajili ya familia.

Ukwaju ni moja ya matunda yanayosifika kwa kutengenezea juisi. Tunda hili lenye wingi wa Vitamin B, C, K na aina nyingine za madini yenye faida mwilini, linaweza kutengeneza juisi tamu, inayofaa kutumiwa kipindi hiki cha jua kali.

Juisi ya ukwaju haina gharama ukilinganisha na aina nyingine ya juisi. Ina mahitaji machache na inafaa sana kwa watu wenye familia kubwa.

Fuatana nami mpaka mwisho wa makala haya ujifunze na kuongeza ujuzi wa kutengeneza juisi ya ukwaju.

Mahitaji

  • Ukwaju nusu kikombe
  • Sukari robo kikombe
  • Iriki
  • Vanilla robo kijiko

Maandalizi

Hatua ya kwanza kwenye uandaaji wa juisi hii ukishanunua ni kuuloweka ukwaju kwenye maji kiasi.

Baada ya dakika 10 anza kuukoroga kwa kutumia mwiko, au kijiko kisha bandika jikoni mpaka uchemke.

Ongeza sukari nusu kikombe au zaidi kutegemea na wingi wa juisi yako

Weka vanila robo kijiko, pamoja na hiriki kama utapendelea.

Baada ya dakika tano sukari ikichanganyika vizuri epua na uchuje kisha ache ipoe.

Ikipoa unaweza kuweka kwenye friji ipate ubaridi kidogo au unaweza kuongeza vipande vya barafu na juisi yako itakuwa tayari kwa kunywa.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV