Jinsi ya kuandaa mafuta ya nazi nyumbani

October 8, 2024 2:38 pm · Mlelwa Kiwale
Share
Tweet
Copy Link
  • Mafuta ya nazi husaidia kuongeza unyevu katika ngozi huku ikisadia kupambana na chunusi na kuponya ngozi iliyoungua.

Nazi ni miongoni mwa viungo maarufu vinavyotumika katika mapishi mbalimbali ikiwemo wali, maharage na aina nyingine za mboga.

Umaarufu wa kiungo hiki unazidi kuongezeka siku za hivi karibuni ambapo hupatikana kiurahisi madukani zikiwa tayari zimeshachujwa na kupakiwa katika pakti maalum.

Mbali na kutumika katika mapishi kiungo hicho hutumika kuandaa mafuta ambayo hung’arisha na kuimarisha ngozi.

Tovuti ya masuala ya afya ya Healthline inaeleza kuwa mafuta ya nazi husaidia kuongeza unyevu katika ngozi huku ikisadia kupambana na chunusi na kuponya ngozi iliyoungua.

Ili kupata faida hizo, unaweza kuandaa mafuta ya nazi nyumbani na kuepukana na gharama ya kuyanunua kila mara.

Utakachohitaji ni nazi (kiasi chako), maji safi,chujio na chombo cha kupikia(sufuria).

Jinsi ya kuandaa

Anza kwa kuandaa nazi, kwa kuzikuna  kwa kutumia kibao au kuzisaga kwa blenda mpaka zitakapokuwa laini.

Endelea kwa kuchuja nazi kwa maji masafi ili kuhakikisha unapata tui zito la kutosha ambalo utaweza kupata mafuta kwa wingi zaidi.

Baada ya kuchuja weka tui katika chombo kisafi na uliache kwa masaa 12 au zaidi. Unaweza kuweka katika friji au sehemu yoyote yenye joto la wastani.

Ili kufahamu kama tui lipo tayari kwa hatua inayofuata utaona limejitenga kwa kutengeneza matabaka mawili la juu likiwa limeganda au kushikana kiasi na chini likiwa maji matupu.

Ukifikia hapo tumia chujio kuondoa maji na ubaki na tui zito lililoganda  kwa ajili ya kuendelea na hatua nyingine.

Endelea kwa kuwasha jiko na kubandika sufuria yenye tui jikoni kisha uache lichemke hadi litakapoanza kutoa mafuta.

Baada ya hapo chuja mafuta kwa chujio au kitambaa kisafi kuondoa makapi yaliyopatikana kisha utayahifadhi katika chombo kisafi kwa ajili ya matumizi.

Mapaka hapo utakuwa tayari umetengeneza mafuta mazuri ya nazi, unaweza kuongeza viungo kama majani au mafuta ya ‘rosemary’ ili kuongeza harufu nzuri.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV