Jack Ma akabidhi mikoba ya Alibaba kwa washirika wake

September 10, 2019 1:23 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link

Anastaafu akiwa anatimiza miaka 55 huku akishikiria rekodi ya kuwa wa kwanza kwa utajiri nchini China kwa utajiri wa Dola za Marekani Bilioni 38.4 (Sh88.3 trilioni) ikiwa ni kwa mujibu wa jarida la Forbes la Marekani. Picha| Mtandao.


  • Nafasi yake kama mwenyekiti wa kampuni ya Alibaba Group imechukuliwa na Daniel Zhang
  • Ataendelea kuwa mwanabodi wa kampuni hiyo hadi kikao cha 2020
  • Utumishi wake unabaki kwenye  ‘Alibaba Partnership’ kwa kipindi chote cha maisha yake.

Dar es Salaam. Mwanzilishi wa kampuni inayojihusisha na manunuzi ya mtandaoni ya Alibaba,  Jack Ma ameachia ngazi rasmi kama Mwenyekiti Mtendaji wa kampuni hiyo.

Amemkabidhi mikoba yake rasmi, Daniel Zhang ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo inayokuwa kasi duniani. 

Ma aliachia ngazi kama Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo mwaka 2018 ambapo alimteua Zhang kukaimu nafasi hiyo na sasa Zhang ana kaimu nafasi ya uenyekiti wa kampuni hiyo.

Hata hivyo, Ma ataendelea kuwa mmoja wa wanabodi wa kampuni hiyo hadi mkutano wa wadau wa kampuni hiyo utakapokutana mwaka 2020.

Ma anabaki kuwa mdau wa “Alibaba Partnership” (kundi la viongozi wa ngazi ya juu wa Alibaba Group) kwa kipindi chote cha maisha yake akihusika katika kutoa mapendekezo yanayohusiana na kampuni hiyo. 

Ma anayeshika nafasi ya 21 katika orodha ya mabilionea duniani, mwaka 2018 wakati anajiaandaa kung’atuka alisema “hii ni ishara kuwa Alibaba inavuka kwenda hatua nyingine ya kiutawala kutoka ngazi ya kampuni inayotegemea mtu binafsi, kwenda juu ya mifumo ya ubora wa shirika na utamaduni wa maendeleo ya talanta.”


Zinazohusiana:


Ma aliachia ngazi kama Mkurugenzi Mtendaji wa Alibaba mwaka 2013 na kukabidhi majukumu hayo kwa Jonathan Lu ambaye pia mwaka 2015 aling’atuka na nafasi hiyo ikashikiliwa na Zhang ambaye alikua Mkuu wa Uendeshaji wa kampuni ya Alibaba Group.

Wakati akimwacha viatu vyake kwa Zhang huku watu mbalimbali wakijadili iwapo viatu hivyo vitamtosha endapo kasi ya soko la biashara ya mtandaoni nchini China itaendelea kusuasua.

Pamoja na majukumu aliyonayo Ma amezidi kuonesha shauku ya kujifunza mambo mbalimbali kwasababu ndicho kitu anachopenda kufanya zaidi katika maisha yake.

Kulingana na ripoti mbalimbali, Ma ni mwalimu mstaafu na mmoja ya waanzilishi wa Alibaba mwaka 1999. 

Anastaafu akiwa anatimiza miaka 55 huku akishikiria rekodi ya kuwa wa kwanza kwa utajiri nchini China kwa utajiri wa Dola za Marekani Bilioni 38.4 (Sh88.3 trilioni) ikiwa ni kwa mujibu wa jarida la Forbes la Marekani. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
17 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
17 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
17 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Siku ya Familia, Mtoto wa Afrika kuadhimishwa Juni 30, 2026

Siku ya Familia, Mtoto wa Afrika kuadhimishwa Juni 30, 2026

Nukta TV

Wadau wa 'kubet" watoa ya moyoni, pendekezo kupanda kwa tozo 5%

Wadau wa 'kubet" watoa ya moyoni, pendekezo kupanda kwa tozo 5%

Nukta TV

Wasemayo wananchi, vocha za kukwangua kupigwa maruku mijini

Wasemayo wananchi, vocha za kukwangua kupigwa maruku mijini

Nukta TV