Instagram yawezesha wafanyabiashara kusaka wateja mtandaoni

December 20, 2019 4:36 am · TULINAGWE ALSON
Share
Tweet
Copy Link
  • Imewawekea kipengele cha “Instagram Business” kinachowasaidia kuwafikia wateja wengi mtandaoni. 
  • Wafanyabiashara wa Tanzania nao wachangamkia teknolojia hiyo kukuza biashara zao.

Ni wazi kwamba mtandao wa instagram umekua moja ya majukwaa ya mtandaoni yanayotumiwa na wafanyabiashara katika kutafuta wateja na kukuza biashara zao katika nchi mbalimbali duniani. 

Wafanyabiashara wengi wamekua wakionyesha bidhaa zao na kupokea oda za wateja kupitia kipengele maalum cha biashara (Instagram business) ambacho kinafanya kazi kama jukwaa la kuwakutanisha wauzaji na wanunuzi wa bidhaa na huduma. 

Instagram imeweka utaratibu huo kwa mfanyabiashara kuonyesha bidhaa yake na kuifanya iwafikie watu wengi kwa muda mfupi na kupata watu wanaoweza kuinunua.

Hata hivyo, huduma hiyo ni kuyalipia kulingana na muda unaotaka kuitangaza bidhaa au huduma yako katika mtandao huo wenye watumiaji takribani bilioni 1 kila mwezi.


ZinazohusianaInstagram yaja na mbinu mpya kudhibiti uzalilishaji mtandaoni


Baadhi ya wafanyabiashara wa Tanzania ambao wanatumia huduma hiyo, wameiambia www.nukta.co.tz imewasaidia kukuza biashara zao kwa sababu wanaweza kuwafikia wateja wengi kwa wakati mmoja bila kutumia gharama kubwa. 

John Dach ni mfanyabiashara wa viatu Jijini Dar es Salaam anasema teknolojia hiyo imemuongezea wateja wengi na kumfanya awe maarufu katika biashara yake ya viatu. 

“Teknolojia hii imenisaidia sana kwa upande wa kupata wateja kwani sikujua kama naweza kutengeneza kundi zuri la wateja kwa muda mfupi,” amesema Dach. 

Huduma kama hiyo inatolewa na mitandao mbalimbali kama WhatsApp na Facebook ambayo ina wafuasi wengi duniani. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
16 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Nukta TV

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Nukta TV

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV