Hisa za Serikali kampuni ya Airtel Tanzania zaongezeka

January 11, 2019 6:52 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link

Rais John Magufuli alipokutana na Mwenyekiti wa kampuni ya Bharti Airtel Sunil Mittal, Ikulu Jijini Dar es Salaam ambapo wamezungumzia maendeleo ya mazungumzo ya umiliki wa hisa za kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania. Picha| Michuzi.


  • Hiyo ina maana kuwa hisa zinazomilikiwa na Bharti Airtel katika kampuni hiyo zimepungua hadi kufikia asilimia 51 kutoka asilimia 60 ambazo ilikuwa inamiliki hapo awali. 
  • Baada ya mazungumzo kukamilika kampuni hiyo kutoa gawio kwa Serikali.

Dar es Salaam. Kampuni ya Bharti Airtel imekubali kuongeza hisa zinazomilikiwa na Serikali katika kampuni ya simu ya Airtel Tanzania kutoka asilimia 40 hadi 49 baada ya kuridhishwa na makubaliano yaliyofikiwa yatakayozinufaisha pande zote mbili. 

Hiyo ina maana kuwa hisa zinazomilikiwa na Bharti Airtel zimepungua hadi kufikia asilimia 51 kutoka asilimia 60 ambazo ilikuwa inamiliki hapo awali. 

Hatua hiyo imefikiwa leo (Januari 11,2019) wakati  Rais John Magufuli alipokutana na Mwenyekiti wa kampuni ya Bharti Airtel Sunil Mittal, Ikulu Jijini Dar es Salaam ambapo wamezungumzia maendeleo ya mazungumzo ya umiliki wa hisa za kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania. 

Mittal amesema kampuni yake imekubali kuongeza hisa zinazomilikiwa na Serikali katika kampuni ya Airtel Tanzania kwasababu kampuni hiyo imeridhishwa na makubaliano yaliyofikiwa yanayolenga kuzinufaisha pande zote mbili na kuboresha huduma za mawasiliano ya kampuni hiyo. 


Inayohusiana: NMB yaingiza sokoni huduma tatu za kidijitali kwa mpigo


Mazungumzo kati ya pande hizo mbili yalianza Machi 12, 2018 baada ya Rais Magufuli kuunda kamati inayoongozwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi ili kutafuta suluhisho la umiliki wa hisa katika kampuni hiyo ya simu nchini.  

Kwa upande wake Rais Magufuli amesema pamoja na kuongeza hisa za Serikali katika umiliki wa Airtel Tanzania, kampuni hiyo imekubali kutoa gawio kwa Serikali mara baada ya mazungumzo hayo kukamilika hapo baadaye. 

“Jambo zuri ni kuwa wamekubali kutoa gawio kwa Serikali ambapo kwa muda wa miaka minane hadi kumi hatukupata, kiasi cha asilimia ya gawio nacho watajadili leo, kwahiyo mimi naona ni mwanga mzuri wa kwenda mbele kwa kampuni ya Barti Airtel na Serikali ya Tanzania pamoja na kampuni zingine,” amesema Rais. 

 Juni 2016, Bharti Airtel pia ilisaini na kuingia makubaliano na Serikali ya kuachia hisa zao za asilimia 35 walizokuwa wakimiliki katika kampuni ya mawasiliano ya Tanzania (TTCL) ambapo sasa kampuni hiyo inamilikiwa na Serikali kwa asilimia 100.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.