Hapo vipi? Magimbi na nyama

September 2, 2022 9:47 am · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Mlo huu unasaidia kuimarisha afya ya ngozi.
  • Ni rahisi kuandaa kama una mahitaji yote ikiwemo nyama na magimbi.

Magimbi ni miongoni mwa chakula kinachopendwa zaidi na watu hasa msimu wa Ramadhani. Hupatikana katika maeneo tofauti tofauti katika mikoa yote ya Tanzania.

Magimbi ni moja ya chakula cha asili kinachotokana na mmea unaoitwa mgimbi.

Imezoeleka kuwa chakula hiki huweza  kupikwa kwa kuchemshwa tu  lakini chakula hiki kinaweza kupikwa kwa namna nyingine tofauti  ya kuvutia na kuweza kuliwa.

Magimbi husaidia katika kuimarisha afya ya ngozi, pamoja na kupunguza hatari kubwa ya kupata magonjwa kama vile kisukari.

MAHITAJI

Nyama iliyochemshwa ½ kilo, magimbi  yaliyo menywa na kukatwa vipande ½ kilo, karoti, pilipili hoho, kitunguu, nyanya, kitunguu  swaumu, nazi,  chumvi, curry powder na pilipili manga.

MAANDAZI

  1. Weka vitunguu kwenye sufuria na vikaange na mafuta mpaka viwe rangi ya kahawia.
  2. Weka vitunguu swaumu, tangawizi mbichi, endelea kukaanga vitunguu visiungue.
  3. Weka Nyanya , subiri ziive, kisha weka karoti pamoja na hoho au pilipili mboga. 
  4. Weka curry powder, kisha weka chumvi kiasi, funika kwa dakika 2.
  5. Weka nyama iliyochujwa maji yote, kisha koroga vizuri ili nyama ichanganyike na viungo vingine.
  6. Kisha weka magimbi, na uweke nazi tui zito lililochanganyika na maji kisha funika mpaka kiive. Baada ya hatua zote magimbi ya nyama yatakuwa tayari kwa kuliwa.
Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Elimu ya kodi mwarobaini wa wafanyabiashara kuikwepa TRA, ianzie shuleni

Elimu ya kodi mwarobaini wa wafanyabiashara kuikwepa TRA, ianzie shuleni

Nukta TV

Rais Samia: Serikali chini ya Magufuli haikutaka kuyumbishwa kukamili kwa JNHPP

Rais Samia: Serikali chini ya Magufuli haikutaka kuyumbishwa kukamili kwa JNHPP

Nukta TV

Rais Samia: Umeme wa SGR hautoingiliwa, Dodoma umeme uhakika 24/7

Rais Samia: Umeme wa SGR hautoingiliwa, Dodoma umeme uhakika 24/7

Nukta TV