Hapo vipi? Magimbi na nyama

September 2, 2022 9:47 am · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Mlo huu unasaidia kuimarisha afya ya ngozi.
  • Ni rahisi kuandaa kama una mahitaji yote ikiwemo nyama na magimbi.

Magimbi ni miongoni mwa chakula kinachopendwa zaidi na watu hasa msimu wa Ramadhani. Hupatikana katika maeneo tofauti tofauti katika mikoa yote ya Tanzania.

Magimbi ni moja ya chakula cha asili kinachotokana na mmea unaoitwa mgimbi.

Imezoeleka kuwa chakula hiki huweza  kupikwa kwa kuchemshwa tu  lakini chakula hiki kinaweza kupikwa kwa namna nyingine tofauti  ya kuvutia na kuweza kuliwa.

Magimbi husaidia katika kuimarisha afya ya ngozi, pamoja na kupunguza hatari kubwa ya kupata magonjwa kama vile kisukari.

MAHITAJI

Nyama iliyochemshwa ½ kilo, magimbi  yaliyo menywa na kukatwa vipande ½ kilo, karoti, pilipili hoho, kitunguu, nyanya, kitunguu  swaumu, nazi,  chumvi, curry powder na pilipili manga.

MAANDAZI

  1. Weka vitunguu kwenye sufuria na vikaange na mafuta mpaka viwe rangi ya kahawia.
  2. Weka vitunguu swaumu, tangawizi mbichi, endelea kukaanga vitunguu visiungue.
  3. Weka Nyanya , subiri ziive, kisha weka karoti pamoja na hoho au pilipili mboga. 
  4. Weka curry powder, kisha weka chumvi kiasi, funika kwa dakika 2.
  5. Weka nyama iliyochujwa maji yote, kisha koroga vizuri ili nyama ichanganyike na viungo vingine.
  6. Kisha weka magimbi, na uweke nazi tui zito lililochanganyika na maji kisha funika mpaka kiive. Baada ya hatua zote magimbi ya nyama yatakuwa tayari kwa kuliwa.
Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa wananchi kupima afya, kuacha uoga

Rais Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa wananchi kupima afya, kuacha uoga

Nukta TV

Uwepo wa vifaa, madaktari uendane na huduma inayotakiwa

Uwepo wa vifaa, madaktari uendane na huduma inayotakiwa

Nukta TV

Rais Samia: Maradhi ya moyo, saratani kwa watoto yaongezeka Tanzania

Rais Samia: Maradhi ya moyo, saratani kwa watoto yaongezeka Tanzania

Nukta TV