Grok yageukia mfumo wa malipo, mataifa waikosoa

January 12, 2026 1:16 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni kufuatia malalamiko makubwa kuhusu matumizi mabaya ya teknolojia hiyo kutengeneza picha za utupu za wanawake na watoto.

Dar es Salaam. Chatbot ya Akili Mnemba (AI) Grok, imeripotiwa kugeukia mfumo wa malipo utakaozuia watumiaji wasiokuwa na alama ya uthibitisho (blue tick) katika mtandao wa kijamii wa X kushindwa kuhariri na kuunda picha.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Januari 10, 2026 kupitia mtandao wa X, Grok inayomilikiwa na mfanyabiashara maarufu Elon Musk itapatikana kwa watumiaji waliolipia pekee suala linalotajwa kupunguza uzalishaji wa maudhui yasiyofaa.

Hatua hiyo imekuja baada ya Grok kukosolewa vikali kwa kudaiwa kutumika kuunda picha za utupu za wanawake na watoto, hali iliyozua taharuki kimataifa na kumuweka Musk katika hatari ya kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwemo faini. 

Uamuzi wa kufanya huduma hiyo kuwa ya kulipia utawalazimu watumiaji wanaotaka kuendelea kutumia huduma hizo kuwasilisha taarifa zao binafsi pamoja na taarifa za kadi za malipo jambo litakalopunguza uundaji wa picha hizo zisizo na maadili.

Mataifa yakosoa uamuzi huo

Pamoja na muelekeo huo mpya wa Grok, viongozi wa kimataifa ikiwemo Ofisi ya Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer imepinga vikali uamuzi huo ikidai hatua hiyo si suluhisho. 

“Kugeuza huduma inayoweza kutengeneza maudhui yasiyo halali kuwa ya kulipia ni dharau kwa waathiriwa wa unyanyasaji na ukatili wa kijinsia,”  imesema Keir Starmer.

Kwa upande wa Umoja wa Ulaya (EU), msemaji wa masuala ya kidijitali Thomas Regnier amesema ni wajibu wa majukwaa husika ikiwemo X kuhakikisha yanazuia kabisa uzalishaji wa maudhui haramu. 

EU pia imeiagiza X kuhifadhi nyaraka na data zote zinazohusiana na Grok hadi mwisho wa mwaka 2026 kutokana na sakata hilo.

Nchi nyingine zikiwemo Ufaransa, Malaysia na India pia zimeikosoa X kwa kushindwa kudhibiti matumizi ya Grok, huku zikitoa wito wa kuwepo kwa udhibiti madhubuti wa teknolojia za AI.

Pamoja na ukosoji huo, Musk ametangaza kuwa mtu yeyote atakayemtumia Grok kutengeneza maudhui ya kinyume cha sheria atachukuliwa hatua sawa na anayechapisha maudhui hayo moja kwa moja mtandaoni.

/
No matches found for this filter
23 May, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
23 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
23 May, 2026
No active movers today
Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MIKOA 5 YA KIPOLISI INAYOONGOZA KWA MAKOSA BARABARANI

MIKOA 5 YA KIPOLISI INAYOONGOZA KWA MAKOSA BARABARANI

Nukta TV

SERIKALI YAKAMILISHA MAZUNGUMZO MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

SERIKALI YAKAMILISHA MAZUNGUMZO MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

Nukta TV

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

Nukta TV