Google kutumia masharti mapya kwa wanaotafuta vitu mtandaoni

February 12, 2020 5:31 am · TULINAGWE ALSON
Share
Tweet
Copy Link
  • Kampuni ya teknolojia ya Google imesema ifikapo Aprili 2020 itasitisha utafutaji wa taarifa zisizotumia mfumo wa (HTTPS) katika vitafutishi vilivyo chini ya kampuni hiyo.
  • Google imesema ni hatua inayosaidia kuweka usalama na usiri wa taarifa za mtu mtandaoni.

Dar es Salaam. Kampuni ya teknolojia ya Google imesema kuanzia Aprili 2020 itaanza kusitisha utafutaji au upakuaji wa taarifa kutika vitafutio vya vitu mtandaoni (Browser)  visivyoendana na kampuni hiyo kwa lengo la kuhakikisha usalama na usiri wa mtu katika kutafuta mambo yake mtandaoni.

Sehemu za kutafutia vitu (Browser)  zinazomilikiwa na kampuni hiyo ni pamoja na Chrome na Mozilla Firefox ambazo hazitaruhusu kupakua taarifa zilizo nje ya utaratibu uliowekwa na Google au zisizotumia anuani ya ya mpangilio unaohakikisha usalama wa taarifa za mtumiaji (https).

Google imeeleza sababu ya maamuzi hayo kuwa ni njia rahisi ya kuweka usalama wa taarifa za wateja wake pamoja na haki ya faragha waliyonayo katika kumiliki taarifa wanazozitafuta bila kuingiliwa na mtu katikati.

Kabla ya hapo ilikuwa rahisi kwa mtu kutumia anuani yoyote kwenye vitafutishi vya Google ambapo ilikuwa inatoa mwanya kwa mtu mwingine  kuingilia kati na kupata taarifa za mtu mhusika.


Zinazohusiana:


Mtaalam wa maswala ya teknolojia Emmanuel Evance anasema hatua hiyo ni nzuri kwani uwezekano wa kuwa na waingiliaji taarifa za watu “Hackers”  utapungua kutokana na kuziba upenyo wa kupata taarifa hizo.

“Mfumo wanaouweka kwa sasa utasaidia sana kuwa na uhuru na taarifa zako kwani ni ngumu mtu kuingilia kati kujua taarifa unazozitafuta mtandaoni kwasababu taarifa zote zitakuwa chini ya mfumo wa http unaoendeshwa na Google wenyewe,”amesema Emmanuel.

/
No matches found for this filter
10 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
10 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
10 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa kiwango cha biashara kati ya Tanzania na Sin

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa kiwango cha biashara kati ya Tanzania na Sin

Nukta TV

Mizinga ya heshima, Rais Samia akimpokea Rais wa Singapore, Ikulu Dar es Salaam

Mizinga ya heshima, Rais Samia akimpokea Rais wa Singapore, Ikulu Dar es Salaam

Nukta TV

Mikakati ya Serikali kuhakikisha walimu wa VETA wanapata ajira na mikopo

Mikakati ya Serikali kuhakikisha walimu wa VETA wanapata ajira na mikopo

Nukta TV