Faida utakazopata ukiimarisha usafi kwenye mgahawa

September 26, 2020 5:07 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Usafi wa mgahawa ni pamoja na kuhakikisha chakula kinachopikwa kinalinda afya za wateja wako.
  • Kutoa huduma nzuri zenye kuzingatia kanuni zote za afya. 

Dar es Salaam. Huenda wafanya biashara wenye migahawa wanajiuliza maswali mengi juu ya upatikanaji wa wateja katika migahawa yao bila kufahamu sababu ndogo ndogo ambazo humfanya mteja ashindwe kurudi pale anapomaliza kupata huduma ya chakula.

Wadau wa migahawa iliyojizolea umaarufu jijini Dar es Salaam wamesema kuwa wateja hawavutiwi na ladha ya chakula pekee kwani wapo ambao huzingatia afya zao na huanza kwa kuangalia usafi wa mgahawa.

Meneja wa mgahawa wa Akemi uliopo Posta Jijini Dar es Salaam Bishanga Kalaule ameiambia Nukta Habari (www.nukta.co.tz) kuwa usafi wa mgahawa una uhusiano wa moja kwa moja na wateja wanaokuja kupata huduma.

“Leo ukipata wateja 100, lengo kuu ni kuhakikisha kuwa 100 wote wanarudi kesho. Endapo mgahawa wako upo katika hali ya kuvutia lazima wataambizana na utapata wateja wengi,” amesema Kalaule.

Ni muhimu kwa wamiliki wa migahawa kufahamu kuwa usafi wa mgahawa siyo tu katika eneo la kuuzia chakula lakini huanzia sokoni wakati wa manunuzi. Je, kuna faida gani zingine za usafi katika mgahawa? Tazama video hii kufahamu zaidi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
13 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Ni changamoto gani zinawakabili vijana wa kitanzania kwa sasa ?

Ni changamoto gani zinawakabili vijana wa kitanzania kwa sasa ?

Nukta TV

Akili Unde (AI) ni suluhu ya habari za uzushi ?

Akili Unde (AI) ni suluhu ya habari za uzushi ?

Nukta TV

KAOMBWE: Mfungwa aliyegeuza gereza kuwa darasa la ujuzi Mwanza

KAOMBWE: Mfungwa aliyegeuza gereza kuwa darasa la ujuzi Mwanza

Nukta TV