Fab Lab kuongeza idadi vituo vya ubunifu Tanzania

March 26, 2019 2:03 pm · TULINAGWE ALSON
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni kituo cha ubunifu wa teknolojia kutoka Ireland ambacho kinakusudia kufungua tawi nchini ili kuwafikia vijana wenye mawazo ya kibunifu.

Taasisi ya Fab Foundation ya nchini Ireland inayomiliki kituo cha kijamii cha Fab Lab inakusudia kufungua tawi Tanzania ikiwa ni hatua ya kuwafikia na kuwasaidia vijana wenye mawazo ya ubunifu wa ujasiriamali kufikia ndoto zao. 

Fab Lab ina vituo vya kijamii 7 nchini Ireland ambapo imejikita katika kusaidia mabadiliko ya kisera katika elimu, mafunzo, maendeleo ya jamii kwa kutumia ujasirimali wa teknolojia. 

Akizungumza katika Wiki ya Ubunifu jijini Dar es salaam, Patrick Colgan mjumbe kutoka taasisi hiyo amesema wameona kuna umuhimu wa kuja Tanzania ikizingatiwa kuwa kuna vijana wanafanya kazi nzuri za ubunifu wa teknolojia na wanahitaji kuendelezwa ili kuifikia jamii kwa upana. 

“Mawazo ya wajasiriamali ni muhimu, hivyo taasisi hiyo imeanzishwa ili kubadili mawazo hayo kua kitu kikubwa kwa jili ya nchi,” amesema Colgan.


Soma zaidi:


Katika kuhakikisha Fab Lab inaingia Tanzania kwa wakati, imeanza mchakato wa utafiti wa jinsi kituo hicho kitakavyojiendesha nchini na kuleta matokeo yaliyokusudiwa. 

Ujio wa Fab Lab nchini itakuwa ni fursa ya nyingine kwa wabunifu kufaidika ikizingatiwa kuwa bado uhitaji wa vituo vya ubunifu bado ni mkubwa na watu wengi hasa wa vijijini hawajafaidika kikamilifu na kazi za ubunifu. 

Ripoti ya utafiti wa mtawanyiko wa vituo vya ubunifu Tanzania (A mapping of Tanzanian hubs and innovation spaces) iliyotolewa Novemba 2018 na Mfuko wa Ubunifu wa Maendeleo ya Watu (HDIF) unaeleza kuwa Tanzania ina vituo vya ubunifu 43 ambavyo vinapatikana katika mikoa tisa tu ya Tanzania bara huku Zanzibar ikiwa na vituo vinne tu.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
26 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
26 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
26 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV