Dk Mpango aitaka jumuiya ya kimataifa ijitathmini utekelezaji wa malengo ya maendeleo

September 24, 2019 10:11 am · TULINAGWE ALSON
Share
Tweet
Copy Link
  • Ameitaka ziwajibika ipasavyo ili kutekeleza Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) ya mwaka 2030. 
  • Ameshauri  pia wadau kufunguka juu ya mambo mbalimbali yanayoendelea katika nchi zao ili kuwaokoa wananchi. 

Dar Es Salaam. Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amezitaka jumuiya za kimataifa ikiwemo Tanzania kuwajibika ipasavyo ili kutekeleza Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) ya mwaka 2030.

Amesema lengo kubwa la uwajibikaji huo ni kutimiza malengo hayo kwa pamoja kwani nchi moja ikishirikiana na nyingine, kuna uwezekano wa kupata kitu kinacholeta maana kubwa kwa jumuiya nzima.

Dk Mpango ametoa wito huo kando ya jukwaa la ngazi ya juu la kisiasa (HLPF) jijini New York Marekani linalotathmini utekelezaji wa malengo hayo kwa nchi wanachama 50 waliojitolea kufanyiwa tathimini ikiwemo Tanzania.

“Ni muhimu jumuiya ya kimataifa itambue kwamba wajibu wa kutekeleza haya malengo ni ya ulimwengu mzima, na hususani baadhi ya nchi ambazo zinaonekana zinavuta miguu hasa katika suala la kupunguza hewa ya ukaa ambayo inatuathiri wote,” amesema Dk Mpango wakati akihojiwa na radio ya Umoja wa Mataifa (UN).


Soma zaidi: 


Dk Mpango amewasihi pia wadau kufunguka juu ya mambo mbalimbali yanayoendelea ili kuwaokoa wananchi na Watanzania juu ya mambo yanayowatatiza na kukwamisha maendeleo katika nchi zao.

“Wafunguke, wasipofunguka ulimwengu wetu huu unazidi kuharibika. Kuna nchi mimi nimeenda hata kupumua ni shida. Yaani unaona kama hewa yote imejaa moshi. Kwa hivyo ni vizuri kila nchi ione dhamana kwamba binadamu tunao wajibu wa kutunza hii dunia ili itutunze,” amesema waziri huyo.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV