Data: Undani kuhusu waliopata mikopo elimu ya juu mwaka 2019-2020
- Tayari HESLB imeshatangaza majina ya wanafunzi takriban 31,000 wa mwaka wa kwanza wamepata mikopo hiyo katika awamu ya kwanza ya mwaka wa masomo wa 2019/20.
Dar es Salaam. Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) hatimaye imeanza kutoa majina ya waliofanikiwa kupata mikopo hiyo katika mwaka wa kwanza wa masomo wa 2019/20 katika awamu ya kwanza.Â
Wanafunzi 30,675 wametunukiwa mikopo hiyo katika awamu hiyo ya kwanza huku awamu ya pili ikitarajiwa kutangazwa hapo Oktoba 25.
Kuna mengi ambayo yanahusu mikopo hiyo muhimu katika kufanikisha ndoto ya elimu ya juu kwa sehemu kubwa ya vijana nchini Tanzania.Â
