Corona: Rais Museveni hajapelekwa Ujerumani kutibiwa

June 28, 2021 11:45 am · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link
  • Amezushiwa kuwa amepata Corona na amepelezwa Ujerumani kutibiwa.
  • Habari hizo hazina ukweli bali ni uzushi.
  • Serikali ya Uganda haijatoa taarifa yoyote kuhusu hali ya rais huyo.

Mwanza. Baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuzushiwa kuwa ameamuru uvaaji wa barakoa iwe suala la lazima na siyo hiari Tanzania, wapotoshaji wameenda mbali zaidi na kumzushia Rais wa Uganda, Yoweri Museveni kuwa ameambukizwa Corona na kukimbizwa nchini Ujerumani kupata matibabu.

Hata hivyo, hakuna taarifa rasmi iliyotolewa na Serikali ya Uganda kuhusu afya ya Rais Museveni na kama amepelekwa nje ya nchi kwa matibabu. Hivyo habari hizo zinazosambaa mtandaoni ni uzushi na hazina ukweli wowote.

Habari hiyo ya uongo dhidi ya Museveni aliyekaa madarakani zaidi ya miaka 30 imetengenezwa kupitia akaunti feki ya Twitter ya shirika la habari ya NTV Uganda na kusambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii ikiwemo WhatsApp.

Habari hiyo inaeleza kuwa Rais huyo amepata maradhi ya Corona na kukimbizwa nchini Ujerumani kupata matibabu huku ikisema daktari wake binafsi, Dk Monica Musenero amethibitisha. 

Nini ukweli wa Habari hiyo?

Habari hiyo haina ukweli kwa sababu imetumia akaunti feki ya NTV Uganda na tayari chombo hicho cha habari kimekanusha kuripoti taarifa hiyo huku kikiwataka wananchi kuipuuza kwa sababu siyo yao. 

 Kutokana na umuhimu na nafasi ya aliyonayo Rais Museveni, vyombo vya habari vya ndani na kimataifa vingekuwa vimeripoti habari hiyo, lakini habari hiyo haijaripotiwa na vyombo vya habari.

Aidha, Serikali ya Uganda na taasisi zake hazijatoa taarifa yoyote kuhusu Rais kuugua na anaendelea na shughuli zake za kikazi kinyume na uzushi unaosambazwa dhidi yake. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
28 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
29 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
29 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Jinsi afya ya akili inavyowatesa wanawake makazini

Jinsi afya ya akili inavyowatesa wanawake makazini

Nukta TV

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV