China haitafungua kituo cha polisi Tanzania

October 20, 2022 9:39 am · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Balozi abainisha hakuna mkataba wa ushirikiano wa kipolisi kati ya China na Tanzania. 
  • Afafanua ni lazima kuwe na makubaliano maalumu yenye malengo mahususi.

Dar es salaam. Watanzania wametakiwa kupuuzia taarifa iliyotolewa na idhaa ya kiswahili ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) kuwa  nchi ya China ina mpango wa kufungua kituo cha polisi barani Afrika ikiwemo Tanzania.

Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki amekanusha madai hayo kwa kueleza kuwa taarifa hiyo iliyonukuliwa kutoka baadhi ya vyombo vya habari nchini Nigeria siyo ya kweli bali ina lengo la kuleta sintofahamu.

“Niwahakikishie hizi ni habari za uongo. Sisi kama Tanzania hatuna mkataba wowote wa mahusiano ya ushirikiano wa kipolisi ambao unapelekea kufungua vituo vya polisi kama ilivyodaiwa, hatujaomba wala wao hawajatuomba,” amesema Kairuki.

Balozi  Kairuki amesisitiza kuwa ni kweli upo utaratibu wa nchi moja kufungua kituo cha polisi kwenye taifa lingile lakini lazima kuwe na makubaliano maalum baina ya mataifa hayo kwa madhumuni mahususi.

“China ina makubaliano na nchi ya Italia ya polisi wake kufanya kazi katika nchi hiyo na dhumuni lake lilikuwa kukidhi mahitaji ya maelfu ya watalii wa China waliokuwa wanaenda kutalii katika jiji la Milan,” amesema.

Aidha Kairuki amesikitishwa na kitendo cha BBC kutumia vyanzo visivyo vya kuaminika kuandika habari zake jambo ambalo linashusha heshima ya shirika hilo kongwe duniani.

Taarifa  iliyochapishwa katika tovuti ya BBC na ukurasa wa mtandao wa Twitter  siku ya jumanne Oktoba 18 mwaka huu ilieleza China imekuja na mpango huo ili kudhibiti vitendo vya kihalifu vinavyofanywa na raia wake katika nchi za Tanzania, Nigeria na Lesotho.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.