CHATI YA SIKU: Asilimia 9.1 ya Watanzania wana kisukari
- Serikali imesema kuwa asilimia 9.1 ya Watanzania wenye umri kati ya miaka 25 hadi 64 wana kisukari.
- Hiyo ni sawa na kusema kati ya watanzania 100 waliopo nchini 9 wanaugua ugonjwa huo hatari kwa sasa.
- Lengo la Serikali ni kupunguza wagonjwa wa kisukari kwa asilimia 28 ifikapo 2025 sambamba na kuhamasisha wananchi kujikinga na ugonjwa huo ambao hugharimu pia fedha nyingi kuutibu.

Dar es Salaam. Wakati Tanzania ikiungana na nchi nyingine duniani leo Novemba 14, 2018 kuadhimisha Siku ya Kisukari Duniani (World Diabetes Day), takwimu zinaonyesha kuwa kuna ongezeko la wagonjwa wa kisukari mwaka hadi mwaka duniani kote.
Tamko la Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu lilitolewa leo kuadhimisha siku hiyo limeeleza kuwa Shirika la Afya Duniani linakadiria kuwa idadi ya watu wenye kisukari imeongezeka kutoka milioni 108 mwaka 1980 hadi kufikia milioni 422 mwaka 2014.
Inakadiriwa kuwa kama hakutakuwa na juhudi za makusudi za kupambana na ugonjwa huu, ifikapo mwaka 2035 kutakuwa na wagonjwa 592 millioni duniani.
Kwa upande wa Tanzania, utafiti wa STEPS uliofanywa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikianana Taasisi ya utafiti wa mgonjwa ya binaadamu (NIMR), na Shirika la Afya Duniani, mwaka 2012 uliohusisha wilaya 50 nchini Tanzania, unaonesha kuwa asilimia 9.1 ya Watanzania wenye umri kati ya miaka 25 hadi 64 wana ugonjwa wa kisukari.
Zinazohusiana:
Serikali kupitia Wizara ya Afya inatumia maadhimisho haya kama sehemu ya kuhamasisha jamii kushiriki katika kudhibiti ugonjwa wa kisukari.
“Lengo letu ni kupunguza wagonjwa wa kisukari kwa asilimia 28 ifikapo 2025. Sambamba na kuhamasisha wananchi kujikinga na ugonjwa wa kisukari, lengo la Serikali ni kuhakikisha tunapanua huduma za kupima na matibabu,” inaeleza sehemu ya ripoti hiyo.
Kaulimbiu ya Maadhimisho ya Siku ya Kisukari Duniani mwaka 2018 ni “Familia na kisukari”.
Latest