Chama ushirika Nyanza chatakiwa kuandaa mikakati ya kujitegemea

April 30, 2020 5:11 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya akingea na watumishi wa Bodi ya Pamba nchini ambapo amewataka kubuni mikakati mipya ya kuongeza uzalishaji wa pamba nchini ili kukidhi mahitaji ya viwanda vya kuongeza thamani ya zao hilo.Tukio hili limefanyika leo jijini Mwanza. Picha| Wizara ya Kilimo.


  • Ni baada ya Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo kutokuridhishwa na utendaji wa chama hicho cha ushirika.
  • Ameagiza mali za chama hicho ambazo zinamilikiwa bila uhalali ziandikishwe kuwa mali za umma.
  • Pia, kiongozi huyo ameagiza bodi ya pamba kuongeza uzalishaji wa zao hilo hadi tani zaidi ya 500000 kwa mwaka ujao.

Dar es Salaam. Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya imekiagiza Chama Kikuu cha Ushirika mkoani Mwanza (Nyanza) kubuni njia muafaka za kujitegemea kiundeshaji kwa kutumia rasilimali nyingi ilizonazo.

Kusaya amesema wizara yake ina lengo la kuiona Nyanza inasimama yenyewe, kuwa ya kisasa na ikijiendesha kibiashara na kuboresha maisha ya wakulima wa mikoa inayolima zao la pamba. 

“Tunataka kuona sasa Nyanza mnakuwa na utendaji unaolenga kujiendesha kibiashara tofauti na ilivyokuwa zamani ili wakulima wa pamba wanufaike na ushirika  kupitia mali zao” amesema Kusaya leo (Aprili 30, 2020) wakati alipofanya kikao na watumishi wa chama hicho na kueleza juu ya kutoridhishwa na hali ya utendaji wa chama hicho.

Kiongozi huyo ameagiza chama hicho kipeleke ripoti yake wizarani ifikapo Mei 15 mwaka huu kwani kina mali nyingi zikiwemo nyumba, maghala na mashamba ambayo kwa sasa hayatumiki kuzalisha mali kwa faida na kuwa mali zingine bado zinamilikwa bila uhalali na baadhi ya watu.

“Watieni moyo wana ushirika ili wawe na imani na Nyanza.Nataka nione mkijitegemea na kuwa leo nilitegemea kusikia ripoti ya mafanikio badala ya kunieleza matatizo ya madeni,” amesema.


Soma zaidi: Wakulima kuuza pamba kwa bei wanayoitaka


Aidha, kiongozi huyo amegusia agizo Waziri Mkuu kuhusu urejeshwaji wa nyumba nane zilizokuwa zikimilikiwa isivyo na watu binafsi litekelezwe kwa nyumba hizo kuwa na hati miliki za umma.

Kaimu Meneja Mkuu wa Nyanza Martha Ndeto amesema tayari nyumba saba zilizokuwa zikimilikiwa kinyume ya utaratibu zimerejeshwa na hati zake zipo kwa Msajili wa Ardhi na kuwa kazi ya kuifuatilia nyumba moja iliyobaki inaendelea.

Ndeto ametaja changamoto zinazokikumba chama hicho kuwa ni pamoja na madeni ambayo hadi kufikia leo, yamefikia Sh4.23 bilioni kutoka kwenye benki, taasisi za Serikali na wafanyabiashara.

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...