Bei ya viazi mviringo yaibua tofauti Mtwara, Rukwa

April 22, 2020 12:53 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Bei ya jumla inayotumika leo Mtwara ni zaidi ya mara mbili ya ile ya Rukwa. 
  • Gunia la kilo 100 la viazi mviringo katika masoko ya mkoani Mtwara linauzwa kwa Sh120,000, wakati masoko ya Rukwa  linauzwa kwa Sh45,000.

Dar es Salaam. Watumiaji wa viazi mviringo hasa kutengeneza chipsi katika Mkoa wa Mtwara leo watalala na maumivu kutokana na bei ya jumla ya zao hilo kuuzwa zaidi ya mara mbili ya bei inayotumika katika Mkoa wa Rukwa. 

Takwimu za mazao makuu ya chakula zilizotolewa na Wizara ya Viwanda na Biashara  leo (Aprili 22, 2020) zinaeleza kuwa gunia la kilo 100 la viazi mviringo katika masoko ya Mtwara linauzwa kwa Sh120,000, wakati masoko ya Rukwa linauzwa kwa Sh45,000.

Hiyo ina maana kuwa bei inayotumika leo Mtwara ni zaidi ya mara mbili  ya Rukwa, jambo linalowafaidisha zaidi wafanyabiashara ambao wamepeleka bidhaa hiyo mkoani humo. 

Bei hiyo inayotumika Mtwara ndiyo bei ya juu huku ya Njombe ikiwa ni ya chini ikilinganishwa na bei zinazotumika katika maeneo mengine nchini.

Viazi mviringo ni miongoni mwa mazao makuu ya chakula ambavyo vimekuwa vikutumiwa kwa matumizi mbalimbali ikiwemo kukaanga chispi ambazo zinapendwa zaidi na mabachela. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
16 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Nukta TV

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Nukta TV

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV