Apple yatangaza kuzifanyia marekebisho simu za Iphone 6S

October 7, 2019 1:26 pm · TULINAGWE ALSON
Share
Tweet
Copy Link
  • Imetangaza hatua hiyo, baada ya kubaini baadhi ya simu hizo zina changamoto ya kuzimika ghafla.
  • Simu hizo ni zile zilizotengenezwa kati ya Agosti 2018 na Oktoba mwaka huu.

Kampuni ya simu ya Apple imetangaza kutoa ofa ya kutengeneza bure simu aina ya Iphone 6S na 6S Plus ikiwa zitapata matatizo ya kuzimika ghafla wakati wa kuzitumia. 

Huduma hiyo itawahusu watumiaji wa Iphone  walionunua simu hizo kati ya Agosti 2018 na Oktoba mwaka huu, baada ya kampuni hiyo ya Marekani kubaini kuwa moja ya kifaa cha simu hizo hakiko sawa. 

Hali hiyo imeiweka Apple katika tahadhari ya lolote linaloweza kutokea kwa wateja wa simu hizo na jinsi wanavyoweza kuwasaidia kutatua changamoto hiyo inayoweza kutokea ikiwemo kufanya matengenezo na kuweka kifaa kipya kupitia programu maalum.  

Ili kupata huduma hiyo, mteja atatakiwa kufuata utaratibu maalum unaopatikana kwenye tovuti ya kampuni hiyo, kisha kuingiza namba ya simu (Serial number) ili kuangalia kama simu yake ni moja ya simu inayohitaji huduma hiyo na kufuata maelekezo mengine yanayofuata.


Zinazohusiana: 


Pia mhusika anaweza kupata huduma hiyo ya matengenezo kwa wakala anaetambulika na Apple, kuweka miadi katika duka lolote linalouza vifaa vya rejareja la iOS. 

Kampuni hiyo imetoa angalizo kuwa matengenezo yoyote yatakayoongezeka zaidi ya tatizo hilo yatakuwa ndani ya gharama za mtu binafsi na siyo kampuni.

Hata hivyo, Apple hawajatoa taarifa zaidi juu ya sehemu yenye tatizo na kitu kinachosababisha simu hiyo kuwa na tatizo hilo.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.