Ahueni, maumivu: Bei ya mchele Katavi, Dar

September 28, 2020 11:34 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Bei ya jumla ya zao hilo katika jiji la Dar es Salaam ni zaidi ya mara tatu ya inayotumika Mpanda ambayo ni Sh70,000. 
  • Wafanyabiashara wa jijini humo kulala na tabasamu. 

Dar es Salaam. Wafanyabiashara wa mchele katika jiji la Dar es Salaam leo watalala na tabasamu baada ya bei ya jumla inayotumika kuuza za hilo ni zaidi ya mara tatu ya ile ya Mkoa wa Katavi.

Mchele ni miongoni mwa mazao makuu ya chakula yanayotegemewa na Watanzania kwa ajili ya matumizi mbalimbali ikiwemo chakula. Mazao mengine ni mahindi, mtama, maharage, viazi mviringo na mihogo. 

Takwimu za mazao makuu ya chakula zilizotolewa na Wizara ya Viwanda na Biashara leo (Septemba 28, 2020) zinaonyesha kuwa gunia la kilo 100 la mchele linauzwa kwa Sh230,000 katika soko la Tandika jijini Dar es Salaam.  

Bei hiyo ya jumla ni zaidi ya mara tatu ya ile ya Sh70,000 inayotumika katika Wilaya ya Mpanda katika Mkoa wa Katavi, jambo linalofaidisha zaidi wafanyabiashara na wakulima wanaouza zao hilo katika jiji hilo. 

Bei inayotumika jijini humo, ndiyo bei ya juu ikilinganishwa na mikoa mingine huku inayotumika Mpanda ndiyo bei ya chini kabisa. 

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...