Pauni, Rand na Yuan zaimarika mwanzo wa juma Agosti 24, 2026
- Watumiaji wa sarafu hizo watalazimika kutoboa mfuko zaidi kulinganisha na wiki iliyopita.
Dar es Salaam. Viwango vya ubadilishaji wa fedha katika Benki ya CRDB na Benki ya NMB vinaonyesha mabadiliko katika baadhi ya sarafu za kigeni dhidi ya Shilingi ya Tanzania mwanzoni mwa wiki hii, ikilinganishwa na viwango vilivyochapishwa Jumatano ya wiki iliyopita, Agosti 19, 2026.
Katika Benki ya CRDB, Pauni ya Uingereza (GBP) imeonyesha ongezeko kubwa miongoni mwa sarafu zilizofuatiliwa, huku benki hiyo ikinunua pauni moja kwa Sh3,459.98 Jumatatu, Agosti 24, kutoka Sh3,432.87 Jumatano, Agosti 19.
Hii ni ongezeko la Sh27.11. Kwa upande wa kuuza, kiwango kimeongezeka kutoka Sh3,732.87 hadi Sh3,759.98.
Benki ya NMB pia imeongeza viwango vya Pauni, ambapo kiwango cha kununua kimepanda kutoka Sh3,382 hadi Sh3,407, huku kiwango cha kuuza kikiongezeka kutoka Sh3,729 hadi Sh3,754.
Rand ya Afrika Kusini (ZAR) nayo imeimarika katika benki zote mbili. CRDB imeongeza kiwango cha kununua Rand moja kutoka Sh153.35 hadi Sh155.31, sawa na ongezeko la Sh1.96, wakati kiwango cha kuuza kimepanda kutoka Sh173.35 hadi Sh175.31.
NMB imeongeza kiwango cha kununua Rand kutoka Sh161 hadi Sh162 na kuuza kutoka Sh181 hadi Sh182.

Kwa Yuan ya China (CNY), CRDB imeongeza kiwango cha kununua kutoka Sh370.12 hadi Sh371.40 na kuuza kutoka Sh415.12 hadi Sh416.40. NMB nayo imeongeza kiwango cha kununua kutoka Sh384 hadi Sh385 na kuuza kutoka Sh423 hadi Sh424.
Hata hivyo, Euro (EUR) imeonyesha mwenendo tofauti kati ya benki hizo. CRDB imepunguza kiwango cha kununua Euro kutoka Sh2,944.54 hadi Sh2,942.83, huku kiwango cha kuuza kikishuka kutoka Sh3,244.54 hadi Sh3,242.83.
Kwa upande mwingine, NMB imeongeza kiwango cha kununua Euro kutoka Sh2,918 hadi Sh2,945 na kiwango cha kuuza kutoka Sh3,192 hadi Sh3,219.
Dola ya Marekani (USD) haijabadilika katika benki zote mbili. CRDB imeendelea kununua Dola kwa Sh2,605 na kuuza kwa Sh2,685, huku NMB ikiendelea kununua kwa Sh2,600 na kuuza kwa Sh2,680.
Kwa upande wa sarafu za kikanda, Shilingi ya Kenya (KSH), CRDB imeongeza kiwango cha kununua kutoka Sh16.94 hadi Sh16.97 na kuuza kutoka Sh23.94 hadi Sh23.97. NMB, hata hivyo, imeendelea na viwango vya Sh17.80 kwa kununua na Sh22.40 kwa kuuza.
Wakati huo huo, viwango vya Shilingi ya Uganda (UGX) havijabadilika katika benki zote mbili. CRDB imeendelea kununua Shilingi moja ya Uganda kwa Sh0.685 na kuuza kwa Sh0.735, wakati NMB imeendelea na Sh0.63 na Sh0.90 mtawalia.