‘Kishumba’: Ndizi, maharage vinaposongwa kama ugali

September 9, 2022 5:39 pm · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Chakula maarufu cha kabila la Wapare.
  • Kinapikwa kwa ndizi na maharage vikisongwa kama ugali.

Kishumba ni moja ya chakula maarufu cha kabila la Wapare wanaopatikana mkoani Kilimanjaro ambacho huliwa mchana na hata asubuhi.

Chakula hiki ni mchanganyiko wa ndizi na maharage ambazo huchanganywa pamoja na husongwa na huwa mzito kama ugali.

Kiasili chakula hiki hupikwa kwenye chungu na jiko la kuni. Kwa sasa unaweza kupikia kwenye sufuria lakini ladha na utamu wake ni ule ule.

Unahitaji kuwa na ndizi, maharage, chumvi, magadi, kitunguu na mafuta ya kupikia.

Maandalizi

Menya ndizi kutokana na idadi ya watu watakaokula pishi lako, kisha zikate vipande vidogo vidogo na uzioshe kwa maji safi na uziweke pembeni.

Chambua maharage, yaoshe na uyabandike jikoni mpaka yaive.

Yakikaribia kuiva weka ndizi, kitunguu, mafuta kidogo, magadi na maji kisha ufunike mpaka ndizi na maharage yaive vizuri.

Zikishaiva ziipue na usubiri zipoe kidogo ili uweze kusonga  mpaka ziwe nzito. Hapo pishi lako litakuwa tayari kwa kuliwa. Unaweza kula asubuhi na chai hata mchana.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV