Dk Mpango: Ongezeni matumizi ya nishati safi

March 13, 2023 2:37 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Atoa agizo hilo kwa wakuu wa wilaya Tanzania. 
  • Nishati hiyo itasaidia kuokoa mazingira.

Makamu wa Rais Dk Philip Mpango amesema wakuu wa wilaya wanatakiwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia katika maeneo yao ili kuongeza kasi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi Tanzania. 

Dk Mpango aliyekuwa akifungua mafunzo maalum kwa wakuu wa wilaya leo Machi 13, 2023 jijini Dodoma amesema dunia inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo mabadiliko ya tabianchi, upotevu wa bayoanuai pamoja na uchafuzi wa mazingira. 

“Kasimamieni matumizi ya vyanzo vya maji na matumizi ya vyanzo mbadala ili kupunguza utegemezi mkubwa wa kuni na mkaa kwa ajili ya kupikia,” amesema Dk Mpango.  

Vyanzo mbadala ni pamoja na matumizi ya nishati ya umemejua, bayogesi, gesi ya majumbani (LPG), jotoardhi na upepo ambavyo haviharibu mazingira. 

“Ili kuwa maendeleo endelevu Waheshimiwa wakuu wa wilaya zingatieni na kuimarisha utunzaji na uhifadhi wa mazingira pamoja na usafi katika maeneo yenu. Toeni hamasa kwa wananchi na hasa vijana ili wawe mstari wa mbele katika kushughulikia uhifadhi ikiwemo kupanda miti,” amesema.  

Hivi karibu Rais Samia Suluhu Hassan akiwa katika mjadala wa kitaifa wa nishati safi ya kupikia jijini Dar es Salaam alisema Tanzania imejiwekea malengo ya kufikia kiwango cha asilimia 80 ya matumizi ya nishati safi na salama ifikapo 2032. 

Dk Mpango amesema ili kufikia lengo hilo, wakuu wa wilaya wanatakiwa kufanya kazi kwa karibu na taasisi za umma na sekta binafsi za nishati ikiwemo Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
12 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV