Njia rahisi ya kupika ‘half keki’

July 18, 2024 1:53 pm · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link
  • Hamira sio lazima kuweka kwenye half kake.
  • Poza mafuta yako kila baada ya mpiko mmoja.

Watu wengi wanapendelea kupika ‘half keki’ kwa sababu ni pishi ambalo halitumii nguvu nyingi katika uandaaji wake. Pia ni rahisi kupika hata kwa mtu anayeanza kujifunza mapishi.

‘Half keki’ ni kitafunwa kinachotengezwa kwa ngano ambacho wengine hukifananisha na maandazi.

Kumbuka tu chakula hiki ni fursa ya biashara na matumizi ya nyumbani kwa sababu bei yake ni kati ya  Sh500 hadi Sh1,000 katika migahawa mbalimbali. 

Hata hivyo, bei hutofautiana kutoka eneo mmoja kwenda eneo lingine. Faida itategemea na eneo unalofanyia biashara na mapenzi ya watu kwa chakula hicho ambacho hutumiwa zaidi asubuhi kwa chai au juisi.  

Tuingie jikoni

Hatua ya kwanza ni kuchanganya unga wa ngano na vitu vyote (kasoro mafuta ya kuchomea) kisha ukande. Hakikisha unakuwa mgumu ila usiwe kama unatengeneza biskuti. 

Baada ya hapo sukuma na ukate maumbo uyapendayo (hakikisha unakata vipande vinene kiasi na sio kama maandazi) 

Hatua inayofuata ni kuziweka sehemu yenye joto na uache ziumuke kwa dakika 20 hadi 30.

Zikiumuka zikaange katika moto mdogo ili ziive mpaka ndani, kisha ziipue na uweke katika chujio ili kuondoa mafuta.

Mpaka hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa na kinywaji chochote.

Vitu vya kuzingatia

  • Hakikisha unatumia vipimo sahihi bila kusahau ‘baking soda’ 
  • Sio lazima kuweka hamira kwenye ‘half keki’
  • Kanda unga wako uwe mgumu hata kidole kishindwe kupenya.
  • Weka half keki zako kwenye mafuta kabla hayajapata moto.
  • Poza mafuta yako kila baada ya mpiko mmoja, (unaweza kuepua ili yapoe au ukaongeza mafuta ya baridi)
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Wabunge waliokwenda Morocco bila kibali kikaangoni , utoro ukiibuliwa bungeni

Wabunge waliokwenda Morocco bila kibali kikaangoni , utoro ukiibuliwa bungeni

Nukta TV

Mfahamu Leonard Mususa Alama ya Ungozi iliyoacha majonzi kwa 'MACEOs' Tanzania

Mfahamu Leonard Mususa Alama ya Ungozi iliyoacha majonzi kwa 'MACEOs' Tanzania

Nukta TV

Bei za mafuta mwezi Juni hizi hapa, dizeli ikipaa kwa Sh85

Bei za mafuta mwezi Juni hizi hapa, dizeli ikipaa kwa Sh85

Nukta TV