Fahamu faida za kula magimbi kiafya

August 13, 2024 7:20 pm · Mlelwa Kiwale
Share
Tweet
Copy Link
  • Husaidia kuupa mwili nguvu na kuimarisha afya ya ubongo.
  • Inashauriwa kula kwa kiasi hususan kwa watu wanaoumwa kisukari.

Magimbi ni miongoni mwa vyakula vilivyopo katika kundi la mizizi ambalo kuna vyakula vingine kama viazi vitamu pamoja na mihogo.

Katika baadhi ya maeneo chakula hiki huliwa sana wakati wa mfungo wa Ramadhani hivyo huwa ni nadra kuonekana wakati wote ingawa katika baadhi ya maeneo upatikanaji wake huwa wa muda wote hasa katika masoko rasmi.

Licha ya kwamba hutumika kama kitafunwa wakati wa kifungua kinywa ambapo humenywa na kuchemshwa tu au katika upishi wa futari ambapo baadhi huyaunga nazi, magimbi yanatajwa kuwa na afya lukuki ambazo mlaji ananufaika nazo.

Makala hii imeangazia faida za kiafya azipatazo mtu anayekula magimbi kwa kurejea maoni ya wataalamu wa afya na lishe.

Huupa mwili nguvu

Magimbi yana madini ya kabohaireti yanayosaidia kuzalisha nishati na kuupa mwili nguvu hivyo yanaweza kutumika kama chanzo kizuri zaidi ya vyakula vya viwandani au vya kukaangwa na mafuta ambavyo havishauriwi sana na wataalamu wa afya.

John Bosco Mkazi wa Mbagala jijini Dar es Salaam ameiambia Nukta Habari kuwa amekuwa akijihisi kuwa na nguvu zaidi anapotumia magimbi kama kitafunwa tofauti na anapokula vyakula vingine kama maandazi au chapati.

“Nikila magimbi huwa nakuwa na nguvu tofauti na vitafunwa vyengine kama maandazi au chapati ambazo hunisababishia kupata njaa, kuliko magimbi ambayo huchukua muda mrefu,” amesema Bosco.

Kauli ya Bosco inaungwa mkono na Dk Stephe Mwenda mtaalamu wa lishe wa kujitegemea ambaye anabainisha kuwa vyakula vya jamii ya mizizi kama magimbi si tu husaidia kuupa nguvu mwili bali kupunguza hatari ya magonjwa ya moyo.

Aina ya virutubisho vinavyopatikana katika magimbi

Kwa mujibu wa Dk. Mwenda magimbi yamesheheni virutubisho lukuki kama vile Kalori, Protini, Nyuzinyuzi, Vitamini C, Vitamini B5, Manganizi’, Magneziamu, Potashiumu pamoja na Kopa ambavyo vina faida kiafya.

Kuimarisha afya ya ubongo

Mtaalamu huyo wa lishe ameongeza kuwa faida nyingine za magimbi ni pamoja na kuimarisha utendaji kazi wa ubongo, husaidia kupambana na baadhi ya saratani pamoja na kuimarisha mfumo wa mmeng’enyo wa chakula.

Hata hivyo, Dk Mwenda ameshauri kuwa, ni muhimu kula chakula hicho kwa kiasi hususan kwa  watu wenye kisukari kwa kuwa husababisha kuongezeka kwa uzito.  

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV