Serikali yaweka mikakati kuwainua mama, baba lishe Tanzania

April 21, 2026 4:00 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni pamoja na kuwapa elimu na ujuzi utakao wasaidia kuboresha kazi zao.

Dar es Salaam. Serikali ya Tanzania imesema inaendelea kuweka mikakati mahususi ya urasimishaji na uwezeshaji wa biashara ndogo ndogo ikiwemo kundi la mama na baba lishe ili wawe sehemu ya utekelezaji wa dira ya 2050.

Ahadi hiyo imetolewa na Rais Samia Suluhu aliyekuwa akizungumza leo katika kongamano la Umoja wa Mama Lishe (UMALITA) lililofanyika jijini Dar es Salaam leo Aprili 21, 2026 akikisistiza kuwa kundi hilo ni miongoni mwa sehemu muhimu nchini likiwezesha makundi mbalimbali ya Watanzania kufanya kazi zao.

Hii ni mara ya kwanza kwa kundi hilo kukutana na Rais Samia baada ya uzinduzi wa mkakati wa Taifa wa matumizi ya nishati safi ya kupikia (2024 2034) ukiliolilenga zaidi kundi hilo ili kuboresha mazingira yao ya kazi kwa kuhamia katika nishati safi ya kupikia.

Pamoja na mkakati huo kuendelea kupiga hatua bado kundi hilo linakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kunyanyaswa na kusumbuliwa ambapo Rais Samia ametaka zikomeshwe haraka.

Awali, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mama na Baba Lishe Tanzania (Umalita), Julieth Malata, ameeleza kuwa, ukosefu wa mitaji na miundombinu mibovu ni vikwazo vikuu vinavyokwamisha ustawi wa sekta hiyo nchini.

Malita ameongeza kuwa upatikanaji wa mikopo yenye masharti nafuu bado ni kitendawili, hali inayowafanya wengi kushindwa kuendeleza biashara zao na kubaki katika lindi la umaskini licha ya mchango wao mkubwa katika uchumi wa nchi.

Aidha, amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan, kusaidia kutatua changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo, ikiwemo unyanyasaji kutoka kwa baadhi ya askari mgambo wakati wa kutoa huduma.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
3 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
3 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Nukta Africa yang’ara tuzo za EJAT 2025, yanyakua tuzo nne

Nukta Africa yang’ara tuzo za EJAT 2025, yanyakua tuzo nne

Nukta TV

Matumizi mabaya ya madaraka bado changamoto Utumishi wa umma

Matumizi mabaya ya madaraka bado changamoto Utumishi wa umma

Nukta TV

Ridhiwani Kikwete achukizwa na tabia hii ya baadhi ya Maofisa Rasilimali Watu.

Ridhiwani Kikwete achukizwa na tabia hii ya baadhi ya Maofisa Rasilimali Watu.

Nukta TV