Kampeni ya ‘Mamalishe na Samia kuchochea matumizi ya nishati safi ya kupikia Tanzania

February 13, 2025 8:09 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Itaanza kufanyika katika wilaya zote za mkoa wa Dar es Salaam na baadae kuifikia nchi nzima.

Mwanamuziki na mama lishe maarufu nchini Zuwena Mohamed (Shilole) amezindua kampeni ya ‘Mamalishe na Samia’ yenye lengo la kuongeza matumizi ya nishati safi kwa wafanyabiashara wanaojishughulisha na kuuza chakula nchini.

Akizungumza katika uzinduzi wa kampeni hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam leo Februari 13, 2025 Shilole amesema kampeni hiyo inalenga kuwapongeza Mama Lishe nchini pamoja na kuwasaidia kwa kuwapa vifaa vya kupikia ambavyo vinatumia nishati safi.

“Mama lishe imekuja kukomboa mama lishe tumtoe kwenye kupikia kuni na mkaa aende kwenye kutumia nishati safi ya kupikia…kila mtanzania anatakiwa kutumia jiko la gesi, umeme pamoja na nishati mbadala,” amesema Shilole.

Kampeni hiyo ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za Rais Samia kuhamasisha matumizi ya  nishati safi ya kupikia ili kufikia asilimia 80 ya watumiaji wa nishati hiyo sawa na iliyoainishwa na Mkakati wa Nishati Safi ya Kupikia uliozinduliwa mwaka 2024.

Ili kufikia lengo hilo, Serikali pamoja na wadau mbalimbali wameendelea kutoa elimu na kusambaza majiko ya nishati safi ikiwemo gesi atika maeneo mbalimbali nchini ili watu wengi zaidi wahamasike kutumia nishati hiyo.

Januari 27 mwaka huu wasanii wa maagizo kutoka Kundi la Lamata na Warembo wa Samia Queens wametoa Mitungi ya gesi 300 kwa Mama Lishe na Baba Lishe katika soko la samaki la feri, lilipo ilala jijini Dar es Salaam lengo ikiwa ni kuongeza watumiaji wa nishati hiyo nchini.

Aidha Shilole amesema kampeni hiyo inatarajiwa kwenda nchi nzima lakini kwa sasa itafanyika katika wilaya za Mkoa Wa Dar es Salaam huku ratiba ya mikoa mingine ikitarajiwa kutolewa siku chache zijazo.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
12 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
12 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
12 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV