Tumia viwango hivi kubadili fedha za kigeni leo Mei 13, 2026
- Leo Dola ya Marekani imenunuliwa kutoka CRDB na NMB kwa wastani wa Sh2,560 na kuuzwa kwa Sh2,640 iliyokuwa ikitumika jana.
Dar es Salaam. Viwango vya ubadilishaji wa fedha za kigeni dhidi ya Shilingi ya Tanzania leo Mei 13, 2026 vimeendelea kuwa tulivu katika baadhi ya sarafu kuu za kimataifa .
Uchambuzi wa viwango vya kubadili fedha za kigeni vya benki kubwa za biashara nchini za CRDB na NMB, unabainisha kuwa Shilingi imeendelea kuwa tulivu dhidi Dola ya Marekani (USD).
Leo Dola ya Marekani imenunuliwa kutoka CRDB na NMB kwa wastani wa Sh2,560 na kuuzwa kwa Sh2,640 iliyokuwa ikitumika jana.
Kwa ujumla, mwenendo wa leo unaonyesha kuwa soko la fedha za kigeni nchini linaendelea kuwa tulivu, huku mabadiliko yanayoonekana yakibaki katika viwango vidogo.
Hali hii inaendelea kuwapa nafuu wafanyabiashara, wawekezaji na wasafiri wanaotegemea fedha za kigeni katika shughuli zao za kila siku, ikiwemo uagizaji wa bidhaa kutoka nje ya nchi, malipo ya ada za kimataifa pamoja na majukumu mengine ya kifedha.

Latest