Fahamu mahitaji ya usingizi kwa watoto wachanga

January 16, 2026 6:51 pm · Goodluck Gustaph
Share
Tweet
Copy Link
  • Usingizi ni muhimu sana kwa ukuaji wa mwili na akili ya mtoto.

Dar es Salaam. Usingizi ni miongoni mwa mahitaji muhimu kwa binadamu, hususan watoto wachanga katika miaka miwili ya mwanzo ya maisha yao.

Tofauti na watu wazima, watoto huhitaji muda mwingi zaidi wa kulala ili kuwawezesha kukua vizuri na kuimarisha uwezo wa ubongo kufanya kazi kwa ufanisi.

Kwa mujibu wa tovuti ya masuala ya afya ya Stanford Medicine Children’s Health, watoto wachanga huhitaji hadi saa 17 za usingizi kwa siku, ambazo hugawanyika katika vipindi mbalimbali.

“Ratiba ya usingizi wa mtoto ni muhimu sana kwa ukuaji wake wa mwili, maendeleo ya akili (kumbukumbu, kujifunza na umakini), udhibiti wa hisia, pamoja na ujuzi wa mwendo wa mwili,” inaeleza tovuti hiyo.

Tovuti hiyo inabainisha kuwa watoto wenye umri wa kuanzia siku moja hadi miezi mitatu ya mwanzo wanahitaji kulala wastani wa saa 16 hadi 17 kwa siku, lakini mara nyingi hawalali zaidi ya saa 1 hadi 2 kwa wakati mmoja.

Aidha, watoto wenye umri wa miezi minne hadi 12 wanahitaji kulala wastani wa saa 12 hadi 16 kwa siku, huku wale wenye umri wa mwaka mmoja hadi miaka miwili wakihitaji kulala kati ya saa 11 hadi 14 kwa siku.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...

Enable Notifications OK No thanks