Silinde awahimiza wakulima, wafugaji Mwanza kujiunga na vyama vya ushirika
- Vyama hivyo vitawawezesha kupata mkopo wa kilimo kwa urahisi.
Mwanza. Naibu Waziri Wizara ya Kilimo, David Silinde amewahimiza wakulima na wafugaji mkoani Mwanza kuanzisha au kujiunga na vyama vya ushirika vya akiba na mikopo vilivyopo kwenye maeneo yao ili kuwaepusha kujiingiza katika mikopo umiza.
Silinde aliyekuwa akizungumza Jijini Mwanza leo Oktoba 21, 2024 ameeleza umuhimu wa wakulima hao kujiunga na vyama vya ushirika ikiwemo kujiwekea akiba na kuepuka mlolongo mrefu wa kupata mikopo kwenye taasisi nyiingine za kifedha.
โNitoe rai kwa wananchi na wakulima kuona umuhimu wa kujiunga na โSaccosโ ili pindi wanapohitaji fedha kwa ajili shughuli za kilimo waweze kupata kwa urahisi kupitia kwenye Saccos zao,โ amesema Silinde.
Aidha, Silinde amewataka viongozi na watendaji wa vyama hivyo vya Saccos kutoa elimu kwa wakulima ili waweze kupata uelewa wa kazi zinazofanyika ili kuwasaidia wakulima wengi kujiondoa kwenye vyama vinavyowaumiza.
Kwa upande wake Dk Benson Ndiege, msajili wa vyama vya ushirika nchini ametaja mafanikio yaliyofikiwa na vyama hivyo ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa amana za wachama kutoka Sh 897 bilioni hadiย kufikia Sh 967 bilioni ukilinganisha taarifa ya mwaka 2022/23
โLakini pia mikopo inayotolewa na vyama vya akiba na mikopo imeongezekaย na kufikia Sh1.11 trilioni kutoka Sh1.05 trilioni pia kuna ongezeko la wananchi kujiunga na vyama hivyo,โ amesemaย Dk Ndiege.

Baadhi ya wananchi na wanachama wa vyama vya ushirika vya akiba na mikopo wakiwa kwenye maadhimisho ya vyama vya ushirika yanayofanyika Jijiji Mwanza. Picha|Mariam John/Nukta.
Naye Hajjat Aziza Mshana,ย Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika wa Akiba na Mikopo Tanzania (Sccurt), amesema vyama hivyo vimeendelea kuimarika katika maeneo mbalimbali ikiwemo kuongezeka kwa mitaji, mali, wanachama na utoaji wa mikopo.
โHivyo ni viashiria vinavyotupa nguvu ya kuendelea kuboresha zaidiย utendaji wa Saccos zetu,โ amesema Hajjat Aziza.
Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Silinde ameagiza vyama hivyo vya Saccos kuacha kujiendesha kwa mazoea kwa kutumia makaratasi badala yake wawekeze kwenye mfumo wa Tehama katika kuboresha utendaji wao.
Latest