Bei ya maharage haishikiki mkoani Dar es Salaam

October 4, 2024 8:00 pm · Yuster Massawe
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam leo ndio wananunua maharage kwa bei ya juu zaidi Tanzania, wakinunua kilo moja kwa Sh3,900 sawa na Sh 390,000 kwa gunia la kilo 100, huku wakazi wa Kigoma wao wakila bata ambapo kwa kilo moja hiyo hiyo ya maharage wao wananunua Sh 1,500 sawa na Sh 150,000 kwa gunia la kilo 100.

Maharage ni mboga pendwa kwa watu wenye kipato cha kati na chini ambayo hutumika kusindikiza mlo kama ubwabwa, chapati au ugali.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Enable Notifications OK No thanks