Wakulima washauriwa kutumia teknolojia ya kisasa ya kilimo cha umwagiliaji

September 18, 2018 5:35 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni kile kinachotumia mfumo wa matone kinachopunguza upotevu wa maji na kuongeza mavuno.
  • Wakulima wengi bado wanalima kilimo cha kienyeji cha umwagiliaji.

Dar es Salaam. Licha ya watanzania wengi kuchangamkia kilimo cha umwagiliaji kama njia ya kujipatia kipato, bado wanakabiliwa na changamoto ya kulima kienyeji ikiwemo matumizi yasiyo sahihi ya maji na miundombinu duni ya umwagiliaji, jambo linalowakwamisha kufaidika na kilimo hicho.

Inakadiriwa kuwa hekta 461,000 sawa na asilimia 5 ndiyo zinatumika kwa kilimo cha umwagiliaji kati ya hekta 29.4 milioni zilizopo kutokana na kilimo cha mazoea na uwekezaji mdogo unaofanywa kwenye sekta hiyo

Hata wakulima wanaolima kienyeji bado wanakabiliwa na changamoto ya matumizi mabaya ya maji ikiwemo upotevu wa kiasi kikubwa cha maji kinachopotea kwasababu ya kukosa miundombinu ya kisasa kusimamia maji na ukuaji wa mazao.

Kutokana na changamoto hizo, kampuni ya vifaa vya umwagiliaji ya Vishakha kutoka India imekuja na teknolojia ya umwagiliaji kwa njia ya matone ambayo inaweza kuwa mkombozi kwa wakulima wa Tanzania wenye nia ya kuendeleza sekta ya umwagiliaji nchini.

Kilimo cha umwagiliaji kinaweza kuboreshwa ikiwa wakulima watapewa teknolojia ya kisasa. Picha| Wikipedia.

Mshauri wa maendeleo ya Biashara kutoka kampuni hiyo, Mayur Parikh amesema teknolojia ya matone inasaidia kuondokana na changamoto za kilimo cha mazoea cha kutumia maji mengi bila kuzingatia mahitaji ya mimea.

“Ni vyema tutumie maji kwa ufanisi katika kilimo cha umwagiliaji kwa maslahi ya kilimo,” amesema Parikh.

Tofauti na mashine zingine za umwagiliaji, mashine za Vishakha humwagilia maji kwa mfumo wa matone hasa kwa mazoa yanayolimwa kwa ukaribu kama miwa, mboga mboga, pamba, ndizi na maua kwa kuunganisha mpira wenye matundu yanayopitisha maji moja kwa moja kwenye shina la mmea.

Kwa kutumia vifaa hivyo, mkulima huweza kutumia kiasi kidogo cha maji kwa siku na hivyo kuepusha gharama za umeme kama anatumia pampu ya kurusha maji shambani. Pia anaokoa muda wa kukaa shambani kwa muda mrefu na kumpa nafasi ya kufanya shughuli zingine za uzalishaji.

Parikh anabainisha kuwa umwagiliaji wa matone unatoa uhakika wa mazao kupata maji ya kutosha na kukua kwa wakati na kumpatia mkulima mazao yanayoendana na gharama za uzalishaji.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
21 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
21 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
21 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Nukta TV

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Nukta TV

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

Nukta TV