Kwanini kuna watumiaji wachache wa pasipoti katika huduma za kifedha?

February 25, 2019 10:38 am · Zahara
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni watu wawili tu kati ya 100 ama asilimia mbili ya watumiaji wa huduma za kifedha waliojiandikisha hutumia huduma hiyo.
  • Watumiaji wa vitambulisho vya kupigia kura ni wengi kuliko vitambulisho vyingine.

Dar es Salaam. Je wewe ni mtumiaji wa pasipoti katika kujiandikisha kwenye huduma za kifedha? Kama ndiyo basi utaingia katika kundi la wachache wanaoitumia pasipoti zao katika kujisajili na huduma hizo .

Hayo yamebainika katika Ripoti ya utafiti wa masuala ya kifedha ya Finscope ya mwaka 2017  FinScope Tanzania 2017 kuliofanywa ati ya Aprili-Julai unaeonyesha kuwa katika fomu wanazopewa wateja kujaza na watoa huduma za fedha wakati wa usajili huwa wanaweka vitambulisho mbalimbali kama alama ya utambulisho.

Ripoti hiyo imeonyesha kuwa katika kufanikisha huduma hizo za kifedha, zaidi ya robo tatu ya watumiaji ama asilimia 83 hutumia vitambulisho vya kura huku asilimia tisa hutumia vitambulisho vya Taifa. Hii ina maana kuwa zaidi ya watumiaji wanane kwa 10 hutumia vitambulisho vya kura kufanya miamala yao huku takriban mmoja tu kati ya 10 hutumia vitambulisho vya Taifa.

Ripoti hiyo inaeleza zaidi kuwa asilimia tatu ya watumiaji hao hutumia vitambulisho vya TASAF (Mfuko wa maendeleo ya Jamii), leseni za udereva (asilimia tano) huku wanaotumia pasipoti katika kufanikisha miamala yao huwa ni asilimia mbili tu.

Takwimu hizi zina maana gani? Ni kweli watanzania wenye pasipoti ni wachache au hawapendi kutumia katika kujiandikishia kwenye huduma mbalimbali za kifedha?

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa wananchi kupima afya, kuacha uoga

Rais Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa wananchi kupima afya, kuacha uoga

Nukta TV

Uwepo wa vifaa, madaktari uendane na huduma inayotakiwa

Uwepo wa vifaa, madaktari uendane na huduma inayotakiwa

Nukta TV

Rais Samia: Maradhi ya moyo, saratani kwa watoto yaongezeka Tanzania

Rais Samia: Maradhi ya moyo, saratani kwa watoto yaongezeka Tanzania

Nukta TV